WAGONJWA 6,847 WATIBIWA HOSPITALI YA WILAYA HANDENI

February 24, 2025


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mohamed Mchengerwa amesema wagonjwa wapatao 6,846 wamepata huduma za Afya Katika Hospitali ya Wilaya ya Handeni tangu ilipokamilika na kuanza kutoa huduma.

Waziri Mchengerwa ameyasema hayo wakati wa uzinduzi wa Hospitali hiyo  iliyozinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa katika siku ya kwanza ya ziara yake mkoani Tanga.

Amesema ujenzi wa hospitali hiyo  umegharimu jumla ya shilingi Bilioni 7.3 ambapo Serikali imetoa kiasi cha shilingi Bilioni 4.3 na wadau wa Islamic Help wametoa kiasi cha shilingi Bilioni 3.

Amesem mpaka sasa jumla ya majengo yaliyokamilika ni 15 amesema Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Mkoani Tanga hadi sasa imeshapokea wajawazito  900 na kati yao  300 walijifungua kwa njia ya upasuaji ndani ya miaka mitatu(3). 

Rais Samia amefanya uzinduzi  wa hospitali hiyo akiwa katika ziara mkoani Tanga ambayo ameanza leo Februari 23, 2025 hadi Machi 1, 2025 kwa lengo la kukagua na kuzindua miradi mbaliambali iliyotolewa fedha na Serikali.





Share this

Related Posts

Latest
Previous
Next Post »