GSM FOUNDATION INABORESHA MBINU ZA UHIFADHI WA TAKA KWA SHULE ZA MSINGI KWA KUGAWA VIFAA VYA KUTUNZIA MAZINGIRA

October 18, 2024

 Katika hatua muhimu ya kukuza utunzaji wa mazingira, GSM Foundation inafurahia kutangaza kupeleka vifaa vya kuhifadhia taka 15 kwa matumizi ya maeneo ya nje ya shule, 25 kwa matumizi ya ndani ya madarasa, na tolori 1 kwa shule ya Msingi Pius Msekwa.

Mpango huu ni sehemu ya ahadi ya kuendelea kuhamasisha elimu ya uhifadhi wa taka na mbinu sahihi miongoni mwa wanafunzi wa shule za msingi nchini kote, na kusaidia serikali katika kutekeleza Mpango Kabambe wa Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (2022-2032) wa serikali yetu ya Tanzania unaojulikana kama Mpango wa Kitaifa wa Kimkakati wa Mazingira (NEMPSI).

Mbali na vifaa hivi vilivyotolewa kwa Pius Msekwa, GSM Foundation hapo awali imeshagawanya na kusanifu jumla ya vifaa 35 vya kuhifadhi taka kwa matumizi ya nje, vifaa 40 kwa matumizi ya darasani na vikwembe vinne kwa shule 2 katika eneo la Kinondoni. Vifaa hivyo vimesaidia wanafunzi 3,144, ambapo 1,633 ni wanawake na 1,511 ni wanaume.

“Mkakati wetu ni zaidi ya utoaji wa vifaa vya kuhifadhi taka; ni kukuza uwajibikaji wa kimazingira kwa watoto wetu, kutoa elimu ya mbinu sahihi za usimamizi wa taka katika utamaduni wa shule, tunalenga kuwawezesha wanafunzi si tu kukubali tabia hizi wao wenyewe, bali pia kuwa mabalozi wa uwajibikaji wa mazingira ndani ya familia zao na jamii zao. Kupitia hili, tunahakikisha kwamba kanuni za usimamizi wa taka endelevu zinapitishwa, zikiunda athari chanya na za kudumu katika jamii,” alisema Bi. Faith Gugu, Kiongozi wa GSM Foundation.

Hii inafanikiwa kupitia kugawa na kuweka matangazo yenye ujumbe wa usimamizi wa mazingira. Mbali na Shule ya Msingi Pius Msekwa, jumla ya matangazo 150 yamegawiwa na kuwekwa katika maeneo mbalimbali ya mashule na katika shule hii pia, matangazo 50 yatawekwa.

Mpango huu unaonyesha umuhimu wa elimu ya mazingira na unawahamasisha wanafunzi na jamii zao kushiriki. Kipengele muhimu cha mpango huu ni faida ya kiuchumi ambayo inaweza kupatikana kwa jamii inayowazunguka. Kwa kukuza uhifadhi sahihi wa taka, jamii zilizo karibu na shule zinaweza kuuza taka zinazoweza kuchakatwa na kutumika kwa matumizi mengine.

“Tunaamini kwamba kila hatua ni muhimu,” aliongeza Faith. “Kwa kufanya kazi pamoja, tunaweza kuleta mabadiliko ya kudumu katika jamii zetu.”

GSM Foundation inaazimia kuendesha mabadiliko ya pamoja katika miradi ya usimamizi wa uhifadhi taka sahihi kwa shule nyingine nchini kote, ikiwa na mpango wa kufanya makabidhiano ya vifaa kwa shule 1 kila mwezi hadi Juni, 2025.






Share this

Related Posts

Previous
Next Post »