RAIS SAMIA NA MGENI WAKE RAIS WA JAMHURI YA GUINEA-BISSAU MHE. EMBALÓ, WASHUHUDIA UTIAJI SAINI WA MKATABA WA MUONGOZO WA USHIRIKIANO

June 22, 2024

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Guinea-Bissau Mhe. Umaro Sissoco Embaló, wakati wakishuhudia utiaji saini wa Mkataba wa Muongozo wa Ushirikiano baina ya Nchi mbili, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 22 Juni, 2024. Kulia ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba akitia saini kwa upande wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa na Jamii wa Jamhuri ya Guinea-Bissau Mhe. Carlos Pinto Pereira akitia saini kwa upande wa nchi yake.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba akiwa pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa na Jamii wa Jamhuri ya Guinea-Bissau Mhe. Carlos Pinto Pereira wakati wakionesha Hati ya Mkataba wa Muongozo wa Ushirikiano baina ya Nchi mbili, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 22 Juni, 2024.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu ziara ya Mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Guinea-Bissau Mhe. Umaro Sissoco Embaló Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 22 Juni, 2024. 
Rais wa Jamhuri ya Guinea-Bissau Mhe. Umaro Sissoco Embaló akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu ziara yake, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 22 Juni, 2024.

(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »