MADEREVA WA MABUS YAENDAYO MIKOANI WAPATIWA HUDUMA YA UPIMAJI MACHO

March 15, 2024


Na Mwamvua Mwinyi,MBEZI Machi 15

Hii ni wiki ya maadhimisho ya Ugonjwa wa Shinikizo la macho au Presha ya Macho duniani ambapo hospitali ya CCBRT,kwa kushirikiana na hospitali ya Barrack PolisI Kilwa Road na halmashauri ya Manispaa ya Ubungo, wameadhimisha kwa kutoa huduma ya upimaji macho kwa madereva wa mabasi yaendayo mikoani kwa lengo la kunusuru uoni wa macho yao kutokana na kazi muhimu wanayoifanya.

Pia huduma hii inatolewa kwa mtu yoyote anayefika kituoni hapo ambapo tangu kuanza kwa zoezi hilo la wiki moja tarehe 12.3.2024 zaidi ya watu 400 walikuwa wamepatiwa huduma.

Ugonjwa wa presha ya macho unatajwa na wataalamu wa afya ya macho duniani kuwa wa kwanza kusababisha upofu usiotibika duniani.





Share this

Related Posts

Previous
Next Post »