PINDA AWATAKA WATANZANIA KUENZI MEMA YA LOWASSA

February 17, 2024

 Na Pamela Mollel,Arusha 

Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo Peter Pinda amewataka watanzania kuendelea kuyakumbuka na kuyaenzi mambo mema aliyoyafanya hayati Edward Lowassa wakati wa uhai wake na kuona namna gani ya kuendelea kuyasimamia yale mema ambayo alikuwa anataka yatekelezwe.

Mhe.Pinda ameyasema hayo wakati akizungumza katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa waziri mstaafu hayati Edward Lowassa iliyofanyika nyumbani kwake katika  kijiji cha ngarash Monduli ambapo amesema hayati Edward Lowassa alikuwa ni kiongozi shupavu na mzalendo wa nchi yake.

Awali akitoa salamu za pole katika msiba huo Mtendaji Mkuu wa Kituo cha Kimataifa Cha AICC Laurence Mafuru amesema kuwa watamuenzi hayati Edward Lowassa kwa kazi kubwa aliyoifanya ya kukuza uchumi na utalii wa mikutano ambayo ndiyo azma ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu ya kuifanya Tanzania kama kitovu cha utalii.

Kwa upande wake Jenista Mhagama Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika na masuala ya sera,bunge na uratibu amesema hayati Edward Lowassa ameacha alama wakati akiwa mtumishi na mtendaji ndani ya serikali kwani matunda na alama aliyoicha inaigusa nchi.

Ameongeza kuwa Serikali itaendelea kuenzi na kutambua mambo mema aliyoyafanya ambapo inaungana na kila mmoja kujifunza kutokana na mifano mema aliyoifanya na kuitenda wakati wa uhai wake.

Naye Mkuu wa chuo cha uhasibu Arusha (IAA)Prof.Eliamani Sedoyeka   anasema atamkumbuka Hayati Edward Ngoyai Lowassa kwa mchango wake mkubwa kwenye sekta ya elimu ambapo aliweza kuanzisha na kusimamia shule za kata kwa nchi nzima

"Kabla ya kujenga shule za kata hapa nchini kulikuwa na shule elfu moja tu,baada ya kujenga tulifanikiwa kupata shule 3500-4000,kwa nchi nzima ukichanganya na shule za binafsi unapata shule 5000"alisema Sedoyeka 

Aliongeza kuwa sasahiv tunawasomi wengi waliopitia shule za kata na wanafanya vizuri,yote hayo ni juhudi za Lowassa.




Share this

Related Posts

Previous
Next Post »