KATIBU WA SUKI AWAONYA WANACCM WENYE KUENEZA SIASA CHAFU KWA VIONGOZI.

February 04, 2024

 NA WILLIUM PAUL, MOSHI.


WANACHAMA wa Chama cha Mapinduzi wameonywa kuachana na tabia ya kufanya siasa chafu ya kuwachafua viongozi waliopo madarakani na Chama kitaendelea kuwalinda viongozi hao.

Hayo yamesemwa leo na Katibu wa Siasa na Uhusiano wa Kimataifa (SUKI) na Mjumbe wa Kamati kuu ya CCM, Rabia Abdallah Hamid wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 47 ya kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Kilimanjaro zilizofanyika kata ya Kindi wilaya ya Moshi.

Alisema kuwa, muda wa kufanya kapeni haunafika kwani Chama kinatambua kwa sasa kinawabunge na madiwani na kuwaonya wale wote wenye nia ya kugombea nafasi hizo kusubiri mpaka muda utakapofika.

"Niwaonye wanaccm kuacha tabia ya kufanya siasa chafu kwa viongozi wetu waliopo madarakani sisi tunawatambua waliopo madarakani na tutawalinda ili watimize wajibu wao na kutekeleza Ilani ya CCM" Alisema Rabia.

Na kuongeza "Wabunge na Madiwani hawana shida ila shida wanaletewa na watu wenye uchu wa madaraka ambao wamekuwa wakifanya siasa chafu za kuwachafua sasa niwaonye wanachama wenye nia hiyo kuacha".





Share this

Related Posts

Previous
Next Post »