ADC KUTOA MIFUKO 100 YA SARUJI KUCHANGIA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI

January 21, 2024

Na Mwandishi Wetu,HANDENI

Katibu Mkuu wa Chama Cha Alliance Demokratic Change ADC) Doyo Hassani Doyo ameshiriki katika mkutano wa kuchagua viongozi wa tawi la Kibaya wilayani Handeni Mkoani Tanga huku akiwahaidi wananchi chama hicho kitashirikiana nao katika suala la maendeleo

Doyo aliyasema hayo wakati kabla ya kuanza uchaguzi huoi ambao pia amewahaidi wananchi kuwa wao kama chama watatoa Mifuko 100 ya Saruji kwa ajili ya ujenzi wa shule ya sekondari kibaya endapo mchakato huo ukiwa sawa .

Alisema kwamba wataanza kutoa mifuko 40 kwanza kisha wakati ujenzi ukiendelea  watamalizia  mifuko 60  iliyobakia lengo likiwa ni kuhakikisha kua sula la maendeleo linafanyika katika eneo hilo .

Hatua hiyo ya ADC kutoa mifuko hiyo ya Saruji ni baada ya wananchi wa eneo hilo kutoa kero juu ya watoto wao kutembea umbali mrefu kwenda shule ya Mzeri na wakatti wa mvua hishindwa kwenye shule kutokana na uchafu wa barabara 

Kutokana na uwepo wa changamoto hiyo wananchi hao waliomba kujengwe shule ya Sekondari maeneo ya karibu ambapo Katibu huyo kupitia chama chao wakahaidi  kuchangia mifuko 100 ya cement kwaajii ya kusapoti mambo ya kijamii.


Share this

Related Posts

Previous
Next Post »