DC MAYANJA AWATUNUKU VYETI WALIOFIKA KILELE CHA MT. HANANG'

October 23, 2023

 


Na John Walter-Manyara

Mkuu wa wilaya ya Hanang'  Janeth Mayanja  amewataka wananchi kujenga tabia ya vivutio vilivyopo ikiwemo kupanda mlima Hanang'  unaopatikana katika wilaya hiyo mkoani manyara.

Ameyasema hayo wakati  aliposhiriki katika zoezi la  kupanda  mlima huo, zoezi lililoandaliwa na wakala wa huduma za misitu Tanzania (TFS) Hifadhi ya mazingira ya Mlima Hanang' ambapo  amesema zoezi hilo litasaidia  vijana kujifunza,kutunza  na  kulinda mazingira hasa katika hifadhi hiyo.

Aidha Mayanja ametoa  vyeti Kwa vijana zaidi 550 kutoka katika maeneo mbalimbali ya Mkoa Manyara ambao wamepanda mlima huo ambao ni wa nne kwa urefu nchini na kuwataka kuwa mabalozi wazuri  wa kutunza na kulinda mazingira katika hifadhi hiyo.

Kwa upande wake Afisa Utalii Katika hifadhi ya Mazingira ya Mlima Hanang'  Elizabeth Mbunda, amesema kutokana na juhudi  mbalimbli za serikali kwa Kushirikiana na wakala wa Misitu Tanzania kuwahimiza na kuona umuhimu wa kutembelea hifadhi, muitikio  wa wananchi  umekuwa mkubwa ikilinganishwa na miaka iliyopita.

Mbunda amesema wenyeji wanaouzunguka mlima huo walikuwa  wanauona  ni kama pori la kawaida lakini baada ya Serikali kuboresha Miundombinu na na kupewa elimu na hamasa Sasa wamekuwa mabalozi wakubwa.

Ameongeza kuwa hifadhi ya mlima Hanang ni zaidi ya Utalii wa Ikolojia ya Mazingira kwani Kuna mimea inayopatikana katika hifadhi hiyo ikiwa ni pamoja na kinyonga anayepatikana mlima huo pekee.

Amesema zoezi hilo la kupanda mlima hufanyika Kila mwaka ifikapo tarehe 14 October siku ya kumbukumbu ya mwalimu Nyerere, lakini mwaka huu hawakuweza kufanya tarehe hiyo kutokana na tukio kubwa  la kuzima mwenge wa Uhuru kitaifa kufanya mkoani humo.

Aidha  amewatoa hofu wazawa juu ya gharama za kupanda mlima na kuona vivutio mbalimbali  kwa kuwa ni rafiki na kila mmoja anaweza kumudu.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »