SERIKALI YAWEKA MSISITIZO MAADILI MAKAO YA WATOTO

September 13, 2023

 



 Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Mwanaidi Ali Khamis akizungumza na Watoto na wasimamizi wa Kituo cha Moyo wa Huruma kilichopo katika Halmashauri ya Mji wa Geita katika ziara yake mkoani Geita 

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Mwanaidi Ali Khamis akitoa zawadi kwa Watoto wa Kituo cha Moyo wa Huruma kilichopo katika Halmashauri ya Mji wa Geita katika ziara yake mkoani Geita.

   


Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Mwanaidi Ali Khamis akikagua mabweni katika Kituo cha Moyo wa Huruma kilichopo katika Halmashauri ya Mji wa Geita katika ziara yake mkoani Geita 

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Mwanaidi Ali Khamis katika picha ya pamoja na Watoto mara baada ya kumaliza ziara yake mkoani Geita 
Picha zote na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini WMJJWM
Na WMJJWM Geita
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe Mwanaidi Ali Khamis amekemea vikali baadhi ya wamiliki wa vituo na Makao ya Watoto wanaoendesha Taasisi hizo kinyume cha taratibu na maadili ya kitanzania.
Akiwa ziarani katika Makao ya Watoto Moyo wa Huruma Mjini wa Geita mapema amesema wamiliki hao wana dhima kubwa ya malezi kwa watoro hivyo, ni wajibu wao kuzingatia maadili.
Mhe. Mwanaidi amesema pamoja na jitihada mbalimbali zinazofanywa na wamiliki wa makao za watoto, bado kuna baadhi ya wamiliki wanaendesha Makao ya Watoto kwa kukiuka taratibu.
Amesema, baadhi ya Makao hayana Programu zinazosaidia kujenga maadili ya Watoto na hivyo kisababisha kuporomoka kwa maadili. 
Ameongeza kuwa Baadhi ya wamiliki wa Makao ya Watoto wanatafuta fedha kwa kuwapiga picha, kuchukua video na kusambaza matangazo kwenye mitandao kwa lengo la kujipatia fedha na misaada kutoka kwa wahisani.
“Jambo hili ni kosa na ni kinyume na Sheria ya Mtoto ya Mwaka 2009. Baadhi ya Makao kuendeshwa bila kuwa na Kamati za Makao zenye jukumu kisheria la kusimamia maslahi ya watoto na kushauri kuhusu utolewaji huduma bora katika makao.” alisema Naibu Waziri Mwanaidi 
Aidha amewataka Maafisa Ustawi wa Jamii nchini kuhakikisha wanatoa elimu kuhusu huduma ya malezi ya kambo na kuasili ili kutoa fursa kwa wananchi wanaokidhi vigezo waweze kupewa watoto hao kisheria 
Naye Mkuu wa Wilaya ya Geita 
Mhe. Cornel Magembe amemuhakikishia Naibu Waziri Mwanaidi kusimamia uendeshaji wa Vituo na Makao ya Watoto katika Wilaya ya Geita ili yafuate taratibu na Sheria zilizopo na kuzingatia maadili ya kitanzania.
Akisoma risala ya Kituo cha Moyo wa Huruma Mkurugenzi wa Kituo hicho Sr. Maria Lauda Kulaya amesema Kituo hicho kinahudumia Watoto 159 ambapo Watoto wote wanapata huduma ya Malezi, elimu, Afya na stadi za kazi.
“Tunatoa shukrani kwa Serikali na wadau mbalimbali na wananchi kiujumla kwa kuendelea kusaidia watoto walioko katika Kituo hiki kwa Hali na mali, tunawaomba waendelee kuwa na moyo huo huo wa utoaji” alisema Sr. Maria
Katika hatua nyingine, Naibu Waziri Mwanaidi ametembelea Kikundi cha wajasirimali Safina na kuwaasa kuwa wabunifu katika utengenezaji wa bidhaa zao ili ziweze kupata soko hasa la kimataifa.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »