CHONGOLO AZUNGUMZA NA WADAU MBALIMBALI WA DEMOKRASIA NCHINI

September 11, 2023

 



Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ndugu Daniel Godfrey Chongolo akizungumza na wadau mbalimbali wa demokrasia nchini, wakiwemo Viongozi wa Vyama vya Siasa, Waandishi wa Habari, Viongozi wa Dini, Viongozi wa Asasi za Kiraia na makundi mengine, waliohudhuria uzinduzi rasmi wa Mkutano Maalum wa Baraza la Vyama vya Siasa na Wadau wa Demokrasia Kutathmini Utekelezaji wa Mapendekezo ya Kikosi Kazi na Hali ya Siasa nchini, uliofunguliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, leo Septemba 11, 2023, jijini Dar Es Salaam.

Mkutano huo unaofanyika kwa siku tatu katika ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) unawashirikisha Wadau wa Demokrasia, wakiwemo Wajumbe wa Baraza la Vyama vya Siasa, Viongozi wa Serikali, Viongozi wa Vyama vya Siasa, Asasi za Kiraia, Mashirika Yasiyokuwa ya Kiserikali, Viongozi wa Dini, Viongozi wa Kimila.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »