TAASISI 13 ZA KIMATAIFA KUANGAZIA HAKIMILIKI ZA ARDHI JIJINI ARUSHA

September 11, 2023

 

Ni mkutano wa Siku tatu unaozikutanisha Taasisi za Kimataifa kutoka mataifa 13 barani Afrika kujadili utekeleza wa hakimilki za ardhi kwa wenyeji wa bara la Afrrika baada ya tafiti kuonesha ongezeko la uelewa wa hakimilki za ardhi hususani kwa wenyeji wa Afrika kusini mwa jangwa la Sahara.

Mkutano huu   ni hatua muhimu ya kimkakati kuendeleza uwajibikaji na hatua zitakazopelekea utekelezaji wa Mkutano wa Kimataifa wa Mazingira wa mwaka 2023 kwa lengo la kuimarisha utashi wa kisiasa, kukusanya rasilimali na kuandaa mpango kazi wa utekelezaji wa hakiardhi barani Afrika.

Mgeni rasmi wa Mkutano huu ni Naibu Waziri Mkuu wa Tanzania na Waziri wa Nishati  Dkt. Doto Biteko, Taasisi zitakazoshiriki katika Mkutano ni pamoja na Mashirika yasiyo ya Kiserikali, Mawaziri wa kisekta kutoka Nchi 13 za Afrika na utafanyika katika hoteli ya Mount Meru ya Jijini Dodoma tarehe 12 Septemba mwaka huu.

Serikali na Taasisi za Kimataifa barani Afrika wanaangazia usalama wa watu na jamii za jadi kama nyenzo muhimu ya amani ya Jamii na maendeleo endelevu ya kiuchumi barani Africa aidha pamoja na juhudi hizi sheria na sera za zilizotungwa miaka 15 iliyopita bado hazijatekelezwa na kuna fursa chache miongoni mwa Taasisi na Taasisi na baadhi ya Mataifa barani Afrika.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »