RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AZINDUA KANISA LA ANGLICAN DAYOSISI YA KATI DODOMA

August 15, 2023




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akivuta utepe pamoja na Askofu wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Central Tanganyika (DCT) Dkt. Dickson Chilongani kuashiria ufunguzi Rasmi wa Jengo la Kitega Uchumi (Safina House) la Kanisa hilo kwenye Sherehe zilizofanyika katika viwanja vya Kanisa Kuu la Roho Mtakatifu Jijini Dodoma tarehe 15 Agosti, 2023. Wengine katika picha ni Mkuu wa Kanisa la Anglikana Tanzania Mhashamu Dkt. Maimbo Mndolwa pamoja na Maaskofu wengine wa Kanisa hilo nchini.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa pamoja na Maaskofu wa Kanisa la Anglikana Tanzania wakati akikata utepe kuashiria ufunguzi Rasmi wa Jengo la Kitega Uchumi (Safina House) la Kanisa hilo kwenye Sherehe zilizofanyika katika viwanja vya Kanisa Kuu la Roho Mtakatifu Jijini Dodoma tarehe 15 Agosti, 2023.
Muonekano wa Jengo la Kitega Uchumi (Safina House) la Kanisa la Anglikana Tanzania, Dayosisi ya Central Tanganyika ambalo limefunguliwa Rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwenye hafla iliyofanyika katika viwanja vya Kanisa Kuu la Roho Mtakatifu tarehe 15 Agosti, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akicheza pamoja na waimbaji wa Kwaya ya Safina wakati wa Sherehe za ufunguzi wa Jengo la Kitega Uchumi (Safina House) la Kanisa hilo lililopo katika viwanja vya Kanisa Kuu la Roho Mtakatifu Jijini Dodoma tarehe 15 Agosti, 2023.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na Askofu wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Central Tanganyika (DCT) Dkt. Dickson Chilongani wakati wa Sherehe za ufunguzi wa Jengo la Kitega Uchumi (Safina House) la Kanisa hilo lililopo katika viwanja vya Kanisa Kuu la Roho Mtakatifu Jijini Dodoma tarehe 15 Agosti, 2023.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »