WAZIRI KIGWANGALLA AMSIMAMISHA KAZI MKUU WA KANDA - PORI LA AKIBA RUKWA KUPISHA UCHUNGUZI KUFUATIA TUHUMA ZA KUJIHUSISHA NA UJANGILI

March 11, 2018


Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
WIZARA YA MALIASILI NA UTALII

Simu Na: +255 026 2321566
Nukushi: +255 026 2321514
Barua pepe: ps@mnrt.go.tz

      
Mtaa wa Kilimani,
Barabara ya Askari,
S.L. P 1351,
40472-DODOMA


MKUU WA KANDA - PORI LA AKIBA RUKWA ASIMAMISHWA KAZI KUPISHA UCHUNGUZI

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dk. Hamisi Kigwangalla (Mb) amemsimamisha kazi Bwana Emmanuel Barabara, Mhifadhi Wanyamapori Mkuu ambaye pia ni Mkuu wa Kanda – Pori la Akiba Rukwa, lililopo wilaya ya Mlele mkoa wa Katavi, kuanzia jana tarehe 10 Machi, 2018 ili kupisha uchunguzi wa tuhuma zinazomkabili.

Dk. Kigwangalla amechukua uamuzi huo kufuatia taarifa za raia wema kuwa Bwana Barabara amekuwa akishirikiana na majangili katika kuhujumu rasilimali za misitu nchini.

Aidha, Waziri Kigwangalla ameagiza iundwe Kamati ya Uchunguzi ili kubaini ukweli wa tuhuma hizo, na endapo mtuhumiwa huyo atakutwa na hatia, hatua kali za kinidhamu ziweze kuchukuliwa kwa mujibu wa sheria na kanuni za Utumishi wa Umma ili iwe fundisho kwa wengine.

Tunatoa onyo kali kwa watumishi wa Wizara wanaojihusisha na vitendo vya uhujumu wa rasilimali za Misitu, Wanyamapori na Malikale kuacha mara moja kwani hatutosita kuchukua hatua kali za kinidhamu kwa yeyote atakayebainika kujihusisha na vitendo hivyo ikiwemo kufukuzwa kazi.

Watumishi wote wa Wizara wanatakiwa kuzingatia sheria, kanuni, taratibu na miongozo mbalimbali iliyowekwa katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku ya uhifadhi wa rasilimali za nchi kwa faida ya kizazi cha sasa na kijacho. 



Dr. Aloyce K. Nzuki
KAIMU KATIBU MKUU
11 Machi, 2018


Share this

Related Posts

Previous
Next Post »