WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI WA LESOTHO ATEMBELEA MRADI WA DART

February 06, 2018
 Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), Bw. Hija Malamla akizungumza katika kikao cha pamoja kati ya wataalamu wa sekta ya barabara nchini na ujumbe wa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi wa Serikali ya Lesotho uliko nchini kwa ziara ya mafunzo.
 Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mabasi yaendayo haraka (DART), Eng. Ronald Lwakatare (aliyesimama) akifafanua jambo kwa ujumbe wa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi wa Serikali ya Lesotho walipotembelea mradi huo.
 Mkuu wa Kitengo cha Manunuzi cha Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), Bw. Lyanga (wa pili kushoto) akiwasilisha mada kwa ujumbe wa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi wa Serikali ya Lesotho walipotembelea ofisi za TANROADS jijini Dar es Salaam.
 Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi wa Lesotho, Mathabathe Hlalele (wa pili kulia) akisisitiza jambo kwenye kikao cha kubadilishana uzoefu kati ya ujumbe wa nchi hiyo na Tanzania.
 Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi wa Lesotho, Mhe. Lehlohonolo Moramotse (wa tatu kulia) akisisitiza jambo akiwa kwenye moja ya Mabasi yaendayo haraka (DART) alipotembelea mradi huo jijini Dar es Salaam. Wa pili kulia ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mabasi yaendayo haraka (DART), Eng. Ronald Lwakatare.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mabasi yaendayo haraka (DART), Eng. Ronald Lwakatare (katikati) akifafanua jambo kwa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi wa Lesotho, Mhe. Moramotse (kulia) alipo tembelea kukagua mradi huo.

Imetolewa na Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »