MSHINDI WA TATU MZUKA AWAANDALIA CHAKULA CHA PAMOJA WATOTO WANAOISHI KWENYE MAZINGIRA MAGUMU

February 13, 2018
Mshindi wa mchezo wa kubahatish wa Tatu Mzuka aitwaye Mrisho Maganga aliyejinyakulia kitita cha shilingi Milioni 22,hivi karibuni amefanikiwa kufanya Dua ya kumshukuru Mungu  pamoja na Watoto wa kituo cha Watoto yatima cha Umra Orphanage Center kilichopo Magomeni.Maganga alisema kuwa aliamua  kufanya Dua pamoja na kula chakula cha pamoja na watoto hao ikiwa ni sehemu ya kumshukuru Mungu kwa kila jambo.Alisema mara baada ya kufanikiwa kuzipata zile fedha ameziingiza kwenye miradi yake aliyokwa ameipanga kuifanya muda mrefu.
Pichani kushoto ni Mwakilishi wa Mchezo wa kubahatisha wa Tatu Mzuka Patronela Nicolaus akiwa pamoja na baadhi ya wadau wa Kituo hicho cha Watoto waishio katika mazingira magumu, Umra Orphanage Center kilichopo Magomeni
-- Ahmad Issa Michuzi Editorial Director P.O BOX 9033, DAR ES SALAAM. issamichuzi.blogspot.com www.michuzijr.blogspot.com othmanmichuzi.blogspot.com Phone:0713 422 313/ 0783 422 313 Tanzania- East Africa.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »