DC TANGA AIPONGEZA FIVE BROTHERS KWA KUANZISHA MASHINDANO YA REDE

February 28, 2018
MKUU wa wilaya ya Tanga ,Thobias Mwilapwa kulia akimkabidhi Kombe la Ubingwa wa Mashindano ya Rede Nahodha wa  timu ya Magomeni Sisters
Mkuu wa wilaya ya Tanga,Thobias Mwilapwa kulia akimkabidhi kombe  mshindi wa pili ambao ni Mkwakwani Baisket
  Mabingwa wa Mashindano ya Rede ambao ni timu ya Magomeni Sisters wakiwa na kombe lao mara baada ya kukabidhiwa na Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa
 Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa akizungumza wakati akifunga mashindano hayo yaliyofanyika kwenye viwanja vya CCM Mkwakwani mjini Tanga
 Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa kulia akimkabidhi Cheti cha kutambua mchango wake katika mashindano hayo Dj
 Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa kulia akimkabidhi Cheti cha kutambua mchango wake katika mashindano hayo Dj Bad Fuvu
 Sehemu ya Majaji wa Mashindano hayo wakiwa kazini
 Mkuu wa wilaya ya Tanga,Thobias Mwilapwa wa pili kutoka kulia akiwa na Muandaaji wa mashindano ya Rede Nassoro Makau kushoto kutoka ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Five kulia ni Katibu Tawala wa wilaya ya Tanga  Faidha Salim
 Timu ya Magomeni Sisters wakiwa kwenye picha ya pamoja na Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa na wageni wengine wakiwemo waaandaaji wa mashindano hayo
 Sehemu ya timu ambazo zilikuwa zikishiriki mashindano hayo wakiwa na mashabiki wakifuatilia mechi ya fainali
MKUU wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa ameipongeza Kampuni ya Five Brothers kwa kuonyesha ubinifu mkubwa kuanzisha mashindano ya mchezo wa rede ambayo imesaidia kurudisha michezo ya zamani iliyokuwa ikipendwa.
Pongezi hizo zilitolewa mwishoni mwa wiki wakati akifunga fainali za mashindano hayo ambapo mshindi wa kwanza alikuwa ni timu ya Magomeni Sisters ambao walizawadiwa fedha taslimu 120,000 kikombe cha mashindano hayo, medali, unga wa ngano kilo 25 na mafuta lita 10.
Huku mshindi wa pili ambao ni Mkwakwani Baisket iliweza kupata kitita cha sh.70,000,medali,ngano kg 5 na mafuta lita 5 ambazo zilitolewa na mgeni rasmi katika mashindano hayo.
Alisema kimsingi uanzishwaji wa mashindano hayo umekuwa ni chachu kubwa kuweza kujenga umoja na mshikamano kwa vijana kuweza kutumia michezo kama sehemu ya kuimarisha miili yao na kujiepusha na vitendo viovu kwenye jamii.
“Ubunifu huu ambao ulionyesha wakati wa michuano hii ya rede ni mzuri na unapaswa kuendelezwa kila mwaka na sisi tutaendelea kuwaunga mkono kwa kuhakikisha yanafanyika kwa waledi mkubwa “Alisema.
Awali akizungumza, Mratibu wa Mashindano hayo kutoka Kampuni ya Five Brothers,Nassoro Makau alisema mchezo wa rede ni miongoni mwa michezo ambayo ilikuwa imesahaulika kwa kipindi kirefu hivyo wakaona wairudishe ili kuweza kuinua vipaji vinavyopatikana kupitia mchezo huo.
“Kwa kweli sisi kama Kampuni ya Five Brothers tumeona na kudhamiria kwa dhati kuona namna ya kurudisha michezo ya asili ambayo  ni pendwa kwa mkoa wa Tanga kwa kuipa thamani kwani mchezo kama ukuti ukuti na rede ni michezo ya asili hivyo tunapoirudisha tunasaidia kurudisha enzi na kuwakumbusha watu mambo mengi “Alisema Makau.
Alisema msimu huu mashindano hayo yalianza February 8 mwaka huu kwa mtindo wa ligi kwa kushirikisha timu 11 za jiji la Tanga na yamesaidia vijana kushiriki kwa kuonyesha vipaji vyao.
Naye kwa upande wake,Mwenyekiti wa Kongamano la Vijana na Balozi wa Vijana Mkoa wa Tanga,Selemani Mssey alisema mchezo huo utasaidia kuondoa vitendo vya umbea na kusutana kwa wasichana.
“Tanga wasichana walikuwa wakiongoza kusuta lakini uanzishwaji wa mashindano hayo utasaidia kuondoa hali hiyo pia kutoa fursa kwao kutumia michezo kama sehemu ya kuimarisha miili yao lakini kupata kipato “Alisema.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »