Waziri Dk. Kigwangalla kufungua onesho la Chimbuko la Binadamu Afrika, Dar

January 22, 2018
Waziri wa Maliasili na Utalii Dk. Hamisi Kigwangalla (MB) anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kesho Januari 23.2018, kwenye uzinduzi wa Onesho la Chimbuko la Binadamu Afrika, tukio ambalo litafanyika majira ya saa 11 jioni katika viunga vya Makumbusho ya Taifa, yaliyopo mtaa wa Shabani Robert, mkabala na Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM).
Akizungumza wakati wa utambulisho wa tukio hilo, Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa, Profesa Audax Mabulla amebainisha kuwa, tayari maandalizi ya onesho hilo yameenda sawa na watu mbalimbali watanatarajiwa kushuhudia tukio ambalo ni la siku moja wakiwemo viongozi wa Serikali na Mabalozi waliopo nchini, na
watalii wanatarajiwa kuhudhuria.
Profesa Mabulla amebainisha kuwa, Vioneshwa vyote katika onesho hilo hapo kesho, vimepatikana hapa Tanzania kutokana na tafiti za kisayansi na vimehifadhiwa Makumbusho ya Taifa.
“Vioneshwa hivi ni pamoja na masalia ya zamadamu, zana za mawe na
masalia ya wanyama walioishi takribani tangu miaka milioni 4 iliyopita. Pia zipo picha za zamadamu na mazingira waliyoishi wakifanya shughuli zao za kila siku.” alieleza Profesa Mabulla.
Kwa upande wake Mratibu kwa upande wa Tanzania Dk. Agness Gidna amesema Onesho limegawanyika katika sehemu kuu nne zikiwemo Makumbusho ya Taifa la Tanzania ikishirikiana na Ubalozi wa Spain Tanzania. Hii ni pamoja na Makumbusho ya Akiolojia ya
Madrid, Taasisi ya Chimbuko la Binadamu (IDEA) Madrid, Chuo Kikuu cha Alcala Madrid na Makumbusho ya CosmoCaixa Barcelona-Spain huku tamasha zima likidhaminiwa na Kampuni ya Simenti ya Twiga.
“Tunawashukuru kampuni ya Twiga Cement kwa kudhamini onesho la Chimbuko
la Binadamu Afrika (The Cradle of Humankind in Africa). Pia kutakuwa na Semina na onesho hili ni matokeo ya tafiti mbali mbali zinazofanyika bonde la Olduvai na Laetoli, Hifadhi ya Mamlaka ya Ngorongoro.” alieleza Dk Agness.
Aidha Dk.Agness ameongeza kuwa, Onesho hilo litakuwa katika pande nne ikiwemo sehemu ya kwanza inahusu ushahidi wa nyayo za zamadamu zilizongunduliwa huko Laetoli mwaka 1978 na mtafiti Dkt. Mary D. Leakey. Nyayo hizo ziliachwa na zamadamu anayeiitwa Australopithecus afarensis na ni ushaidi usiopingika wa zamadamu kutembea
wima kwa miguu miwili takribani miaka milioni 3.6 iliyopia.
Sehemu ya pili inahusu hadithi ya kusisimua ya kuwa binadamu (Genus Homo) ambapo kuna masalia ya zamadamu Zinjanthropus au Paranthropus boisei na Homo habilis, zana za mawe za mwanzo (Oldowan) zilizotumika katika kujipatia chakula na ushahidi wa kale wa ulaji wa nyama katika historia ya mabadiliko ya binadamu, takribani miaka million 2 iliyopita.
Sehemu ya tatu inahusu maisha ya jamii ya Homo erectus. Jamaii hii inafanana zaidi na binadamu wa sasa kuliko jamii zilizotangulia. Kuna masalia ya zamadamu Homo erectus, zana za mawe (Acheulian) na ushahidi wa ulaji wa wanyama wakubwa kama vile tembo na nyati wa zamani takribani miaka million 1.7 iliyopita.
Sehemu ya nne inaonesha kipindi cha mwanzo cha binadamu wa sasa (Homo sapiens) walioanza kutokea hapa Afrika miaka laki 2 iliyopita. Kuna masalia ya Homo sapiens na zana za mawe za muhula wa kati na muhula wa mwisho.
Mbali na onesho hilo, pia waandaji hao wa Makumbusho ya Taifa inawakaribisha watu wote kuhudhuria semina na ufunguzi wa onesho la Chimbuko la Binadamu Afrika.
Kwa upande wa Semina ambayo inatarajia kuanzia majira ya saa tisa kamili itaendeshwa na watafiti wa Kimataifa, akiwemo Prof. Manuel Dominguez-Rodrigo wa Chuo Kikuu cha Complutense, Spain; Prof. Audax ZP Mabulla na Dk. Agness Gidna.
Na Andrew Chale
Waziri Dk. Kigwangalla kufungua onesho la Chimbuko la Binadamu Afrika, Dar




Waziri wa Maliasili na Utalii Dk. Hamisi Kigwangalla (MB) anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kesho Januari 23.2018, kwenye uzinduzi wa Onesho la Chimbuko la Binadamu Afrika, tukio ambalo litafanyika majira ya saa 11 jioni katika viunga vya Makumbusho ya Taifa, yaliyopo mtaa wa Shabani Robert, mkabala na Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM).
Akizungumza wakati wa utambulisho wa tukio hilo, Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa, Profesa Audax Mabulla amebainisha kuwa, tayari maandalizi ya onesho hilo yameenda sawa na watu mbalimbali watanatarajiwa kushuhudia tukio ambalo ni la siku moja wakiwemo viongozi wa Serikali na Mabalozi waliopo nchini, na
watalii wanatarajiwa kuhudhuria.
Profesa Mabulla amebainisha kuwa, Vioneshwa vyote katika onesho hilo hapo kesho, vimepatikana hapa Tanzania kutokana na tafiti za kisayansi na vimehifadhiwa Makumbusho ya Taifa.
“Vioneshwa hivi ni pamoja na masalia ya zamadamu, zana za mawe na
masalia ya wanyama walioishi takribani tangu miaka milioni 4 iliyopita. Pia zipo picha za zamadamu na mazingira waliyoishi wakifanya shughuli zao za kila siku.” alieleza Profesa Mabulla.
Kwa upande wake Mratibu kwa upande wa Tanzania Dk. Agness Gidna amesema Onesho limegawanyika katika sehemu kuu nne zikiwemo Makumbusho ya Taifa la Tanzania ikishirikiana na Ubalozi wa Spain Tanzania. Hii ni pamoja na Makumbusho ya Akiolojia ya
Madrid, Taasisi ya Chimbuko la Binadamu (IDEA) Madrid, Chuo Kikuu cha Alcala Madrid na Makumbusho ya CosmoCaixa Barcelona-Spain huku tamasha zima likidhaminiwa na Kampuni ya Simenti ya Twiga.
“Tunawashukuru kampuni ya Twiga Cement kwa kudhamini onesho la Chimbuko
la Binadamu Afrika (The Cradle of Humankind in Africa). Pia kutakuwa na Semina na onesho hili ni matokeo ya tafiti mbali mbali zinazofanyika bonde la Olduvai na Laetoli, Hifadhi ya Mamlaka ya Ngorongoro.” alieleza Dk Agness.
Aidha Dk.Agness ameongeza kuwa, Onesho hilo litakuwa katika pande nne ikiwemo sehemu ya kwanza inahusu ushahidi wa nyayo za zamadamu zilizongunduliwa huko Laetoli mwaka 1978 na mtafiti Dkt. Mary D. Leakey. Nyayo hizo ziliachwa na zamadamu anayeiitwa Australopithecus afarensis na ni ushaidi usiopingika wa zamadamu kutembea
wima kwa miguu miwili takribani miaka milioni 3.6 iliyopia.
Sehemu ya pili inahusu hadithi ya kusisimua ya kuwa binadamu (Genus Homo) ambapo kuna masalia ya zamadamu Zinjanthropus au Paranthropus boisei na Homo habilis, zana za mawe za mwanzo (Oldowan) zilizotumika katika kujipatia chakula na ushahidi wa kale wa ulaji wa nyama katika historia ya mabadiliko ya binadamu, takribani miaka million 2 iliyopita.
Sehemu ya tatu inahusu maisha ya jamii ya Homo erectus. Jamaii hii inafanana zaidi na binadamu wa sasa kuliko jamii zilizotangulia. Kuna masalia ya zamadamu Homo erectus, zana za mawe (Acheulian) na ushahidi wa ulaji wa wanyama wakubwa kama vile tembo na nyati wa zamani takribani miaka million 1.7 iliyopita.
Sehemu ya nne inaonesha kipindi cha mwanzo cha binadamu wa sasa (Homo sapiens) walioanza kutokea hapa Afrika miaka laki 2 iliyopita. Kuna masalia ya Homo sapiens na zana za mawe za muhula wa kati na muhula wa mwisho.
Mbali na onesho hilo, pia waandaji hao wa Makumbusho ya Taifa inawakaribisha watu wote kuhudhuria semina na ufunguzi wa onesho la Chimbuko la Binadamu Afrika.
Kwa upande wa Semina ambayo inatarajia kuanzia majira ya saa tisa kamili itaendeshwa na watafiti wa Kimataifa, akiwemo Prof. Manuel Dominguez-Rodrigo wa Chuo Kikuu cha Complutense, Spain; Prof. Audax ZP Mabulla na Dk. Agness Gidna.
Na Andrew Chale,
Waziri wa Maliasili na Utalii Dk. Hamisi Kigwangalla (MB) anatarajiwa kuwa mgeni rasmi hiyo kesho Januari 23.2018.
Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa, Profesa Audax Mabulla akizungumza na waandishi wa Habari (Hawapo pichani) wakati wa utambulisho wa tukio hilo linalotarajiwa kufanyika kesho Januari 23.2018.
 Balozi wa Spain nchini, Bw. Felix Costales akizungumza katika tukio hilo mapema leo Januari 23,2018. Kulia kwake ni  Mkuu wa Makumbusho ya Taifa, Profesa Audax Mabulla
Tukio hilo likiendelea 
Mratibu kwa upande wa onesho hilo kwa Tanzania, Dk. Agness Gidna akionesha maandalizi kwa wanahabari (hawapo pichani) namna itakavyokuwa hapo kesho wakati wa tukio
Baadhi wanahabari wakiangalia Vioneshwa ‘visukuku’ wakati wa tukio hilo la utambulisho 
Vionesho ambavyo vinatarajiwa kuwapo kesho katika tukio hilo
Afisa kutoka ubalozi wa Spain akipata maelezo kutoka kwa Mratibu upande wa Tanzania Dk. Agness Gidna  wa Makumbusho ya Taifa. Kulia ni Balozi wa Spain Bw. Felix Costales 
Afisa kutoka ubalozi wa Spain akipata maelezo kutoka kwa Mratibu upande wa Tanzania Dk. Agness Gidna  wa Makumbusho ya Taifa. Kulia ni Balozi wa Spain Bw. Felix Costales 
Vioneshwa kinachoelezea hatua za binadamu wa kale katika makumbusho ya Taifa ikiwa katika maandalizi ya mwisho mwisho kwa ajiri ya kesho
Vioneshwa kinachoelezea hatua za binadamu wa kale katika makumbusho ya Taifa
Vioneshwa ambavyo vinatarajiwa kuwepo kesho.
Moja eneo la bango la Chimbuko la Binadamu wa Kale. (Picha zote na Andrew Chale)









--

Andrew Chale

Blogger Personality | Journalist | Activist | Online Editor dewjiblog | Comedian |Volunteer Red Cross | Sauti za Busara & ZIFF Festivals 2007 to present.

Telephone: +255222122830 Fax: +255222126833
Golden Jubilee Towers, Ohio Street,20th Floor
Po Box 20660, Dar es Salaam,Tanzania

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »