HALMASHAURI YA WILAYA YA MUHEZA YATANGAZA NEEMA KWA WAKULIMA WA VIUNGO,MACHUNGWA NA MKONGE

June 21, 2025


Na Oscar Assenga, MUHEZA


Halmashauri ya Wilaya ya Muheza,imewatangazia Neema kubwa ,Wakulima wa Machungwa na Matunda aina ya Machungwa,

Neema hiyo kubwa inakuja wakati ambao Kilimo cha mazao hayo kikizidi kukua wilayani humo.


Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri hiyo Dkt.Jumaa Mhina aliwaambia Waandishi wa Habari, wakati wa hafla ya kuwaaga Madiwani wa Halmashauri hiyo iliyofanyika leo wilayani humo,

Dkt Mhina amesema ,wawekezaji wameshaanza kujitokeza kwaajili ya kujenga viwanda na baadhi ya viwanda vitatangazwa hivi karibuni,

"Tayari tumepokea wawekezaji ambao wameshajenga viwanda vya usindikaji wa mazao ya viungo vya chai na sasa mazao hayo yamepanda thamani ambapo karafuu,imepanda kutoka 6,000 hadi 20,000 kwa kg moja ,hivyo hivyo kwa mazao mengine ni hivyo kama pilipili manga,midarasini na Iriki,mazao yote haya yamepanda juu sana kwenye soko" Aliongeza Dkt.Mhina


Kuhusu Zao la Machungwa na Mkonge,Dkt.Mhina alisema,mazao hayo kwasasa kuna Uwekezaji mkubwa unakuja na utatangazwa hivi karibuni, alisema kwasasa kuna kiwanda kinachojihusisha na usindikaji wa maganda ya Machungwa kimeanza kufanya kazi, nakwamba wawekezaji wengine wameshaanza kujitokeza kwaajili ya kufanya Uwekezaji,

"kuhusu za Machungwa, tayari viwanda vya usindikaji vimeshaanza kazi hasa kiwanda Cha kusindika maganda ya Machungwa, lakini pia wawekezaji wengine wameshaanza kujitokeza,

kwa upande wa Mkonge,kilio cha mitambo ya kisasa aina ya korona kuchakata Mkonge wa daraja la 1,2,3,4 ,hadi mwishoni mwaka huu kila kitu kitakuwa tayari na tutawangazia hivi karibuni" Alisisitiza Dkt.Mhina


Kwaupande wake, Mwenyekiti anayemaliza muda wake katika Halmashauri hiyo,Erasto Mhina, amesema,kwakipindi cha miaka mitano wamejitahidi kutekereza miradi mbalimbali katika Wilaya hiyo ikiwemo kuwainua Wakulima wa Mazao ya Kimkakatati kwakuwatafutia masoko makubwa ambayo yamesaidia kuinua uchumi wa Wakulima,

" Uchumi wa wakazi wengi wa Muheza unategemea zaidi Kilimo hasa cha Machungwa na Viungo vya chai,tumejitahidi sana kutekereza miradi hii ya Kilimo na sasa Tunapereka nje ya nchini" Aliongeza Mhina

MWISHO

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »