WAZIRI MAKAMBA AWASILISHA TAARIFA KWA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA KATIBA NA SHERIA

November 02, 2017
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba  (wa pili kushoto)hii leo amewasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Kamati ya Pamoja  ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ya kushughulikia masuala ya Muungano kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria.  Kutoka kulia ni Naibu Katibu Mkuu Bi. Butamo Kasuka Phillip na Katibu Mkuu Mhandisi Joseph Malongo. Kushoto ni Mkurugenzi Idara ya Muungano Bw. Baraka Baraka.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Katiba na Sheria Bi. Najma Murtaza Giga (kulia) akiongoza kikao cha Kamati yake wakati wa uwasilishaji wa taarifa ya utekelezaji wa Kamati ya pamoja ya masuala ya Muungano. Kushoto ni Bw. Dunford Mpelumbe Katibu wa Kamati.


Sehemu ya wajumbe wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria wakifuatilia majadiliano mara baada ya kuwasilishwa kwa taarifa ya utekelezaji wa Kamati ya pamoja ya masuala ya Muungano.

Sehemu ya watumishi wa Ofisi ya Makamu wa Rais wakifuatilia majadiliano katika kikao hicho
 

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »