Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL), hii hapa tena wikiendi hii.
Mechi moja inachezwa kesho Ijumaa Novemba 3, 2017 kwenye Uwanja wa 
Majimaji mjini Songea ambako mwenyeji Majimaji FC itacheza na Stand 
United ya Shinyanga.
Mchezo huo wa Songea utaanza saa 10.00 jioni (1600h).
Jumamosi kutakuwa na michezo mitano ambako minne itaanza saa 10.00 jioni (1600h) wakati mwingine utakuwa saa 1.00 usiku (1900h).
Michezo hiyo ya Jumamosi itakuwa ni kati ya Singida United 
itakayocheza na Young Africans kwenye Uwanja wa Namfua mkoani Singida 
wakati Tanzania Prisons itakuwa wageni wa Kagera Sugar kwenye Uwanja wa 
Kaitaba  mjini Bukoba, Kagera.
Njombe Mji kwa upande wake watakuwa wenyeji wa Mbao FC ya Mwanza 
kwenye Uwanja wa Sabasaba mkoani Njombe huku Mtibwa Sugar ikisafiri 
kutoka Morogoro kwenda Mtwara kucheza na Ndanda FC kwenye Uwanja wa 
Nangwanda Sijaona. Hizo ni mechi zitakazochezwa saa 10.00 jioni.
Mchezo pekee utakaofanyika saa 1.00 usiku utakuwa ni kati ya Azam FC na Ruvu Shooting kwenye Uwanja wa Azam.
Jumapili kutakuwa na michezo miwili ya Ligi Kuu ambako Lipuli ya 
Iringa itakuwa mwenyeji wa Mwadui FC ya Shinyanga kwenye Uwanja wa 
Samora wakati Simba itakuwa mgeni wa Mbeya City kwenye Uwanja wa Sokoine
 jijini Mbeya. Mechi hizo zitaanza saa 10.00 jioni.
 

 
EmoticonEmoticon