RAIS DKT. MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA PROF. IBRAHIM GAMBARI MJUMBE MAALUM WA RAIS WA NIGERIA, CHATO MKOANI GEITA.

January 10, 2017
gm
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na kumkaribisha  Profesa Ibrahim Gambari ambaye ni Mjumbe maalum wa Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari aliyefika Chato mkoani Geita kwa ajili ya mazungumzo.
gm-1
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na Profesa Ibrahim Gambari ambaye ni Mjumbe maalum wa Rais wa Nigeria Chato mkoani Geita.
gm-2
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea barua yenye ujumbe maalum kutoka kwa Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari uliowasilishwa na Profesa Ibrahim Gambari ambaye ni Mjumbe maalum wa Rais huyo wa Nigeria, Chato mkoani Geita.
gm-3
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimsindikiza mgeni wake Profesa Ibrahim Gambari ambaye ni Mjumbe maalum wa Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Chato mkoani Geita.
gm-4
Profesa Ibrahim Gambari ambaye ni Mjumbe maalum wa Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari  akimshukuru Rais Dkt. John Magufuli mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Chato mkoani Geita.
gm-5
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimsikiliza mgeni wake Profesa Ibrahim Gambari ambaye ni Mjumbe maalum wa Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Chato mkoani Geita.
gm-6
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na mgeni wake Profesa Ibrahim Gambari ambaye ni Mjumbe maalum wa Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Chato mkoani Geita. PICHA NA IKULU.
………….
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 10 Januari, 2017 amekutana na kufanya mazungumzo na Mjumbe Maalum wa Rais wa Nigeria Profesa Ibrahim Gambari nyumbani kwake Chato Mkoani Geita. Mazungumzo yao yalilenga masuala mbalimbali ya uhusiano kati ya Tanzania na Nigeria.
Rais Magufuli amempongeza Rais Muhammadu Buhari kwa jitihada kubwa anazochukua kwa ajili ya kuleta maendeleo nchini mwaka.
Pia, Rais Magufuli amempongeza Rais Buhari kwa jitihada anazozifanya za kukabiliana na kundi la Boko haramu ili kuhakikisha amani inaendelea kudumu nchini mwake.
Kwa upande wake Mjumbe Maalum wa Rais wa Nigeria, Profesa Ibrahim Gambari amempongeza Rais Magufuli kwa ushindi alioupata na jitihada anazochukua katika kupambana na rushwa na kubana matumizi jambo ambalo linaungwa mkono na wananchi wengi wa Nigeria.
Profesa Gambari alimkabidhi Rais Magufuli barua yenye ujumbe maalum kutoka kwa Rais Muhammadu Buhari wa Nigeria.

Jaffar Haniu
Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Chato, Geita
10 Januari, 2017

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »