WANANCHI WA KISIWANI PEMBA WATAKIWA KUKABILIANA NA ATHARI ZA MABADILILI YA TABIA NCHI.

June 04, 2016
 Pichani Wataalamu kutoka Ofisi ya Makamu wa Raisi Muungano na Mazingira na Idara ya Mazingira ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar wakiwa ndani ya boti kuelekea mkoa wa kusini Pemba kushiriki zoezi la uzinduzi wa kupanda miti ya mikoko (leo) Juni 4
 Kushoto Naibu wa Waziri wa Wizara ya Nishati, Maji na Mazingira wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Juma Makungu Juma, akimueleza jambo Naibu Waziri wa Mazingira na Muungano Mhe. Luhaga Mpina (katikati) walipokuwa wakielea kupanda miti ya mikoko kisiwa panza kusini Pemba. Kulia ni Muwakilishiwa mkuu wa Wilaya.
Walioinama (kulia) ni Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina akipanda mbegu za miti ya mikoko katika eneo la kisiwa Panza ikiwa ni siku ya uzinduzi wa upandaji miti hiyo kisiwani Pemba, kushoto ni Afisa Mazingira mkuu kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira bw. Cretus Shengena (Picha na Habari zote na Evelyn Mkokoi).

Evelyn Mkokoi,Pemba
4/6/2016

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Joelson Mpina (Mb) amewataka wananchi wa kisiwa Panza katika Mkoa wa Kusini Pemba, kukabiliana na athari zitokanazo na mabadiliko ya tabia nchi kwa kutunza mazingira hasa kwa kupanda miti ya mikoko kwa wingi,ili kunusuru kisiwa hicho kumezwa kutokana na kuongezeka kwa kina cha bahari.
Mhe. Mpina ameyasema hay leo kisiwani Pemba alipozingua kampeni maalum ya kupanda miti ya mikoko ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kitaifa wa kupanda miti.
Awali Mhe. Mpina alisemakuwa, serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania  imeweza kupata kiasi cha fedha shilingi milioni 165 maalum kwa kuhimili athari zitokanazo na mabadiliko ya tabia nchi kwa kujenga kuta za fukwe za Ocean Road jijini Dar es Salaam,Pangani Mjini Tanga, Kilimani mjini unguja na kisiwa Panza kisiwani Pemba.
Aliongeza kuwa, kiasi hicho cha fedha pia kimeanza kutumika katika kampeni hiyo ya kitaifa ya  kupanda miti kwa kupanda miti ya mikoko katika eneo la kisiwa Panza na ambapo miti zaidi ya milioni Moja inatarajiwa kupandwa katika eneo la hekta 238, kisiwani pemba, pamoja na zoezi hilo kuzinduliwa leo kisiwani pemba, miti hiyo aina  ya mikoko pia inatarajiwa kupandwa katika maeneo ya kilimani mjini unguja,bwawani,tovuni, micheweni na Rufiji.
Naibu Waziri Mpina aliongeza kwa kusema kuwa suala la mazingira si suala la Muungano lakini serikali hizi mbili zimeona umuhimu wa kushirikiana katika eneo hili ili kuweza kukabiliana kikamilifu na madhara na hasara zitokanazo na athari za mabadiliko ya tabia nchi ili kunusuru visiwa hivi kumezwa na bahari.
Akitolea mfano wa shule ya msigi na sekondari kisiwapanza  ambazo zipo hatarini kumezwa,  mhe Mpina aliongeza kuwa  wataalam wa masuala ya mazingira watafanya tathmini kikamilifu na kuona namna gani serikali inaweza kuongeza mbinu zaidi za kushughulikia maeneo haya hatarishi, ili maji ya bahari yasiweze kuingia katika maeneo ya makazi.
Naibu Waziri Mpina aliwasisitizia wananchi wa kisiwa panza kutunza  mazingira kwa kutokukata miti ovyo na kuchoma misitu na watunze na kuilinda miti ya mikoko iliyopandwa ili kuweza kufikia dhamira ya kukinusuru kisiwa icho kumezwa.
Kwa upande wake Naibu Waziri wa Mazingira kutoka katika wizara ya Ardhi,Maji,Nishati,na Mazingira wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe.Juma makungu Juma amesema maeneo mengi ya Zanzibar yaliyopo pembezoni mwa bahari yameharibiwa na shughuli za binadamu, hivyo upandaji wa miti ya mikoko katika maeneo hayo utazuia adhari za mabadiliko ya tabia nchi kwa makazi ya watu na mashamba ambayo yamepelekea watu kuanza kuhama katika makazi yao na haya yote ni matokea ya vitendo vya wananchi.
Zoezi hilo la kupanda miti ya mikoko lililofanyika kisiwani pemba limeenda sambamba na maadhimisho ya siku ya mazingira duniani ambayo hufanyika tarehe tano Juni kila mwaka.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »