Elimu ya udereva wa kujihami yawafikia madereva wa TBL Arusha na Moshi

June 13, 2016

VIK1 
Katika kuhakikisha  madereva wanaosambaza bidhaa za kampuni wanafanya kazi zao kwa ufanisi,kampuni ya TBL Group imeandaa mafunzo maalumu kwa madereva kutoka viwanda vyake vilivyopo katika mikoa ya Dar es Salaam,Arusha,Moshi,Mbeya na Mwanza.
Mafunzo hao ambayo yamemalizikia mkoani Arusha yaliendeshwa na mkufunzi wa madereva kutoka kampuni ya CFAO Motors,Hubert Kubo ambaye amewapatia madereva hao elimu  ya udereva wa kujihami ikiwemo utunzaji wa vifaa wanavyoviendesha.
Baadhi ya madereva waliohudhuria mafunzo hayo walishukuru mwajiri wao kwa kuwapatia mafunzo mbalimbali kuhusiana na kazi yao ambayo walidai yanawawezesha kufanya kazi yao kwa ufanisi na kuwa na  uwezo wa kukabili changamoto mbalimbali za kikazi kwa urahisi.
VIK2 
Madereva wakifuatilia mafunzo yaliyokuwa yanatolewa na Mkufunzi Hubert Kubo yaliyofanyika Arusha
VIK3 
Madereva wakifuatilia mafunzo yaliyokuwa yanatolewa na Mkufunzi Hubert Kubo yaliyofanyika Arusha
VIK4 VIK5 VIK6

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »