MCHEZO MGUMU, CITY INANAFASI: REDONDO

March 02, 2016


DSC_0136
Kiungo mshambuliaji wa City, Ramadhani Chombo Redondo amesema  mchezo wa ligi kuu ya soka Tanzania dhidi ya Simba uliopangwa kuchezwa jumapili hii kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar utakuwa mgumu kutokana na mazingira ya timu zote mbili.
Akizungumza  na mbeyacityfc.com mapema leo, Chombo amesema kuwa City inakwenda Dar kucheza mchezo huo ikiwa na kumbukumbu ya kupoteza mchezo wa uliopita kama ilivyo kwa simba, jambo ambalo linaufanya mchezo huo kuwa mgumu kutokana na uhitaji wa matokeo kwa timu zote.
“Ni wazi utakuwa mgumu, hii ni kwa sababu kila timu inahitaji matokeo baada ya kupoteza mchezo uliopita,Simba na timu nzuri na wako kwenye nafasi nzuri pia lakini wasitegeme kupata ushindi kw sababu sisi tunauhitaji zaidi yao” alisema.
Aidha Chombo aliweka wazi kuwa City ina nafasi kubwa ya kufanya vizuri kwenye mchezo huo hasa ukizingatia  kuwa imekuwa na historia nzuri kila inapokutana na Simba kwenye uwanja wa Taifa.
“City imeshinda mara  kadhaa mbele ya Simba,hili ni jambo nzuri kisaikolojia kwa sababu linaleta kujiamini,imani yangu kubwa dakika 90 za jumapili zitakuwa upande wetu” alisema.
Kuhusu ligi kuu ya Vodacom inayoendelea sasa Redondo aliweka wazi kuwa imekuwa ngumu na yenye changamoto nyingi sana,hasa ukizingatia kuwa timu nyingi zilijiandaa vizuri toka mwanzo wa msimu ingawa pia suala la kusima simama au kupanguliwa kwa ratiba linapunguza msisimko wake.
DSC_0084

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »