Waziri wa Afya ,Maendeleo ya
Jamii,Jinsia,Watoto na Wazee Mhe. Ummy Mwalimu akipokea vifaa kutoka kwa
Mkurugenzi wa Bohari ya Dawa yaTaifa Lauren Rugambwa Bwanakunu
vitakavyotumika katika wodi ya Afya ya uzazi ya Mama na Mtoto katika
Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wa pili kushoto ni Kaimu Mkurugenzi
Hospitali ya Muhimbili Prof Lawerence Mseru na nayefata ni katibu Mkuu
wa wizara hiyo Mpoki Ulisubisya .
Waziri wa Afya ,Maendeleo ya
Jamii,Jinsia,Watoto na Wazee Mhe. Ummy Mwalimu akielekezwa jambo katika
nyaraka na katibu Mkuu wa wizara hiyo Mpoki Ulisubisya katika Kitengo
cha Afya ya uzazi ya Mama na Mtoto katika Hospitali ya Taifa ya
Muhimbili.
Baadhi ya vijana wa Jeshi la
Kujenga Taifa (JKT) na mfanyakazi wa Bohari Kuu ya dawa ya taifa (MSD)
walishusha baadhi ya magodoro na vitanda vitakavyotumika katika wodi ya
Afya ya uzazi ya Mama na Mtoto katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Waziri wa Afya ,Maendeleo ya
Jamii,Jinsia,Watoto na Wazee Mhe. Ummy Mwalimu akisaidiana na mmoja wa
kijana wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kubeba boksi lenye takataka
kwenda kuyatupa sehemu husika wakati wakifanya usafi katika jengo
ambalo liliamriwa na Mhe Rais liwe wodi ya Afya ya uzazi ya Mama na
Mtoto katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Waziri wa Afya ,Maendeleo ya
Jamii,Jinsia,Watoto na Wazee Mhe. Ummy Mwalimu akizungumza na Zuhura
Abubakari mmoja ya wagonjwa waliohamishiwa kwenye wodi mpya ya Afya ya
uzazi ya Mama na Mtoto katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Mafundi
wakifunga vitanda katika wodi mpya ya Afya ya uzazi ya Mama na Mtoto
katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Picha na raymond Mushumbusi
MAELEZO.
……………………………………………………………………………………………………………………………..
Na Raymond Mushumbusi MAELEZO
Waziri wa Afya ,Maendeleo ya
Jamii,Jinsia,Watoto na Wazee Mhe. Ummy Mwalimu amepokea vifaa
vitakavyotumika katika wodi ya Afya ya uzazi ya Mama na Mtoto katika
Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ikiwa ni agizo la Mhe.Rais alililolitoa
mapema mwishoni wa wiki iliyopita katika kuhakikisha kuwa wakinamama
wanaojifungua hawalali chini.
Akipokea vifaa hivyo Mhe. Ummy
Mwalimu amesema anamshukuru sana Mhe Rais kwa kuona changamoto hii ya
wakina mama kulala chini wakati wakitoka kujifungua na kumuahidi Mhe.
Rais kusilimamia vyema suala hilo na kuwaagiza wakurugenzi husika kumpa
taarifa ya kuhusu vitanda na magodoro katika Hospitali zote zilizo chini
ya wizara yake.
“ Kuanzia sasa sitolala na natuma
salamu kwa Wakuu wa Mikoa na Wilaya kuwa fursa hii ni wajibu wao kutoa
taarifa kuhusu maendeleo ya afaya hasa katika vifaa hususan vitanda na
magodoro ili kupunguza tatizo hili la wagonjwa katika Hospitali zetu
kulala chini wakati tuna uwezo wa kupata vitanda na magodoro”
‘”Mhe.Rais amenifundisha na
ametufundisha sote kwamba kutatua jambo sio mpaka mkae vikao au semina
ili kujadili ila inawezekana kama mkiweka nia ya kulifanya jambo hilo na
kuachana na zile kauli za tunalifanyia kazi, tupo katika michakato na
kauli kama hizo zisizotatua tatizo kwa wakati unaotakiwa”alisema Ummy.
Bohari ya Dawa ya Taifa
imekabidhi jumla ya vitanda 120, Magodoro 120, Mashuka 480, vitanda vya
kuzalishia 10,vitanda 10 vya kulaza watoto ambao hawajatimia Njiti na
jumla ya vifaa vyote vina thamani ya shilling Million 100.
Uaandaaji wa wodi hiyo ya akimama
wanaojifungua katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili umekuja baada ya
agizo la Mhe.Rais Dkt John Pombe Magufuli alilolitoa hivi karibuni
alipokuwa akiongea na wazee wa Mkoa wa Dar es Salam na kutoa siku mbili
kwa wizara Ya Afya kuhamisha ofisi zilizokuwepo za kitengo Afya ya uzazi
ya Mama na Mtoto na kuifanya kuwa wodi ya akina mama ili kupunguza
tatizo la kulala chini kwa akina mama wanaotoka kujifungua.