Rais wa Jamhuri ya Muungano ya
Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mkuu wa mkoa wa Dar es
salaam Mh. Meck Sadik wakati alipowasili kwenye ukumbi wa Diamond
Jubilee tayari kwa kuongea na wazee wa mkoa wa Dar es salaam leo ambapo
mkutano huo pia ulihudhuriwa na Makamu wa Rais Mama Samia Hassan Suluhu
na Waziri Mkuu Mh. Majaliwa Kassim Majaliwa.
Askofu wa Kanisa la Ufufuo na
Uzima, Josephat Gwajima amehudhuria katika mkutano huo ambapo alionekana
mtu mwenye kufurahia hotuba hiyo, Kamera ya Fullshangwe ilimnasa askofu
huyo maarufu kwa matamshi yake ya “Wakale Malimao” akiwa na tabasam
kubwa akionekana kufurahia kuhudhuria kwake katika mkutano huo.
Mwanzo wakati alipofika ukumbini
hapo alikuta ratiba inaendelea hivyo ilibidi akae viti vya nyuma lakini
Shekh Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Sheikh Alhadi Mussa Salim alimpigia
simu na kumwambia aende mbele akakae pamoja na viongozi wenzake wa dini
na ndipo alipoenda kukaa eneo hilo.
(PICHA NA JOHN BUKUKU- FULLSHANGWE-DAR ES SALAAM)
Msafara wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli ukiwasili kwenye ukumbi wa
Diamond Jubilee leo wakati alipoongea na wazee wa mkoa wa Dar es salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano ya
Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mwenyekiti wa Wazee wa
mkoa wa Dar es salaam mzee Hemed Mkali kutoka kulia ni Mkuu wa mkoa wa
dar es salaam Mh. Raymond Mushi na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es
salaam Ndugu Ramadhan Madabida.
Rais wa Jamhuri ya Muungano ya
Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mwenyekiti wa wazee wa
mkoa wa Dar es salaam wa zamani Mzee Idd Simba, Kulia ni mfanyabiashara
Abdullah Mohamed.
Rais wa Jamhuri ya Muungano ya
Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akizungumza na Waziri Mkuu wa Jamhuri
ya Muungano ya Tanzania Mh. Majaliwa Kassim Majaliwa.
Rais wa Jamhuri ya Muungano ya
Tanzania Dk. John Pombe Magufuli, Makamu wa Rais Mama Samia Hassan
Suluhu na Waziri Mkuu Mh. Majaliwa Kassim Majaliwa na Mke wa Rais Mama
Janet Magufuli wakiwa meza kuu pamoja na viongozi mbalimbali wa mkoa wa
Dar es salaam.
Baadhi ya mawaziri wa wizara mbalimbali katika serikali ya awamu ya tano wakiwa katika mkutano huo.
Baadhi ya viongozi wa dini ya Kikristo na ya Kiislamu wanaounda kamati ya Amani wakiwa katika mkutano huo
Askofu wa Kanisa la Ufufuo na
Uzima, Josephat Gwajima hakubaki nyuma na yeye amehudhuria katika
mkutano huo na hapa akionekana mwenye furaha na bashasha kama
alivyonaswa na kamera yetu.
Askofu wa Kanisa la Ufufuo na
Uzima, Josephat Gwajima akiwa amekaa pamoja na viongozi wenzake wa dini
katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es salaam wakati Rais Dk.
John Pombe Magufuli alipozungumza na wazee wa mkoa wa Dar es salaam.
Baadhi ya wazee wa Dar es salaam wakitambulishwa katika mkutano huo.
Baadhi ya mawaziri waliohudhuria
katika mkutano huo kutoka kulia ni Mh. Profesa Sospeter Muhongo, Dk.
Abdallah Posi, Nape Nnauye, Januari Makamba na Ummy Mwalimu.
Baadhi ya wazee wakifuatilia kwa
makini wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe
Magufuli alipokuwa akihutubia mkutano huo.
Makamu wa Rais Mama Samia Hassan Suluhu akisalimia wazee katika mkutano huo.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mh. Majaliwa Kassim Majaliwa akisalimia wazee katika mkutano huo.
Mwenyekiti wa Wazee wa mkoa wa
Dar es alaam Mzee Hemed Mkali akihutubia katika mkutano huo na
kumkaribisha Rais Dk. John Pombe Magufuli ili kuwahutubia wazee hao.
Wazee hawa wakionekana kuhamasika na hotuba ya Rais Dk. John Pombe Magufuli.
Rais Dk. John Pombe Magufuli akihutubia katika mkutano huo uliofanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee leo.