Mchezaji Thaban Kamusoko amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa Ligi
Kuu ya Vodacom kwa mwezi Disemba, 2015 baada ya kumshinda mchezaji
mwenzake wa Yanga (Amissi Tambwe).
Kamusoko ameisaidia timu yake ya Yanga katika michezo iliyochezwa
mwezi Disemba kwa kushiriki dakika zote katika michezo mitatu
iliyochezwa mwezi wa Disemba.
Kwa kuchaguliwa kwake kuwa mchezaji bora wa wa mwezi Disemba,
Kamusoko atakabidhiwa zawadi ya fedha taslimu shilingi milioni moja
(1,000,000) kutoka kwa wadhamini wa ligi Kampuni ya simu za mkononi ya
Vodacom.