Harakati
za kubomolewa kwa jengo la ghorofa 16 lililoko kwenye Mtaa wa Indira
Gandi jijini Dar es Salaam zinaendelea huku baadhi ya barabara na njia
zinazopita kwenye eneo la jengo hilo zikiwa zimefungwa ilikupisha ujenzi
huo.
Modewjiblog
imetembelea eneo hilo ikishuhudiwa kwa harakati za ubomoaji huo
ukiendelea huku baadhi ya nyumba na maduka yaliyopo karibu na jengo hilo
wakiwa wamepisha na kufunga makazi yao. Taarifa za ubomoaji wa jengo
hilo zinaeleza kuwa zitachukua muda mrefu kutokana na kuwa ubomoaji wake
ambao unaanzia juu kabisa ya ghorofa utachukua muda.
Jengo hilo la ghorofa 16 linavyoonekana kwa mbali (katikati) kama lilivyopigwa pigwa picha mchana wa leo na Andrew Chale wa modewjiblog.com