VODACOM FOUNDATION YANOGESHA UZINDUZI WA MAADHIMISHO YA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO LEO

December 08, 2015


 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni A.C.P Camillus Wambura(kushoto)akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Rosalynn Mworia alipowasili ofisini kwake akiwa kama Mgeni rasmi wa Uzinduzi wa Maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili dhidi ya wanawake na watoto leo katika viwanja vya Polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya Askari polisi na wanafunzi wa Shule ya Msingi Oysterbay na Mbuyuni wakiwa wamebeba mabango yenye ujumbe maalum wakati wa maandamano ya amani ya uzinduzi wa maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili dhidi ya wanawake na watoto leo katika viwanja vya polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam. Uzinduzi huo ulidhaminiwa na Vodacom Foundation.
 Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Oysterbay na Mbuyuni wakiwa wamebeba mabango yenye ujumbe maalum wakati wa maandamano ya amani ya uzinduzi wa maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili dhidi ya wanawake na watoto leo katika viwanja vya polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam. Uzinduzi huo ulidhaminiwa na Vodacom Foundation.
 Askari wa jeshi la polisi kikosi maalum cha Kurasini jijini Dar es Salaam akiongoza maandamano ya amani ya uzinduzi wa maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili dhidi ya wanawake na watoto leo katika viwanja vya polisi Oysterbay.Uzinduzi huo ulidhaminiwa na Vodacom Foundation.
  Baadhi ya Askari polisi na wanafunzi wa Shule ya Msingi Oysterbay wakiwa wamebeba mabango yenye ujumbe maalum wakati wa maandamano ya amani ya uzinduzi wa maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili dhidi ya wanawake na watoto leo katika viwanja vya polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam. Uzinduzi huo ulidhaminiwa na Vodacom Foundation.
 Askari wa jeshi la polisi kikosi maalum cha kutuliza ghasia(FFU)cha jijini Dar es Salaam akiongoza maandamano ya amani ya uzinduzi wa maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili dhidi ya wanawake na watoto leo katika viwanja vya polisi Oysterbay.Uzinduzi huo ulidhaminiwa na Vodacom Foundation.
 Kamishina Msaidizi wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni A.C.P Emanuel J. Mley akiongea na wageni waalikwa waliofika katika uzinduzi wa maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili dhidi ya wanawake na watoto leo katika viwanja vya polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam,Kulia kwake ni Mgeni rasmi wa maadhimisho hayo,Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mawasiliano wa Vodacom Tanzania,Rosalynn Mworia.Uzinduzi huo ulidhaminiwa na Vodacom Foundation.
 Mgeni rasmi wa Uzinduzi wa Maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili dhidi ya wanawake na watoto,Kaimu Mkurugenzi mkuu wa Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania,Rosalynn Mworia akiongea na wageni waalikwa waliofika katika uzinduzi huo leo katika viwanja vya Polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam,Kushoto kwake ni Kamishina Msaidizi wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni A.C.P Emanuel J. Mley.Uzinduzi huo ulidhaminiwa na Vodacom Foundation.
 Mkuu wa Dawati la Jinsia la Polisi Chuo kikuu cha Dar es Salaam,S.P Leah Mbunda(kushoto)akiteta jambo na Mgeni rasmi wa Uzinduzi wa Maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili dhidi ya wanawake na watoto,Kaimu Mkurugenzi mkuu wa Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania,Rosalynn Mworia(kulia) wakati wa maadhimisho hayo,katika ni Mkaguzi msaidizi wa Polisi anayeshughulikia Dawati la Jinsia katika Kituo cha Polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam,A/INSP Prisca Komba.

Kamishina Msaidizi wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni A.C.P Emanuel J. Mley(kulia)akijadiliana jambo na Mgeni rasmi wa Uzinduzi wa Maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili dhidi ya wanawake na watoto,Kaimu Mkurugenzi mkuu wa Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania,Rosalynn Mworia,Wakati wa maadhimisho hayo yaliyofanyika leo katika viwanja vya Polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam na kudhaminiwa na Vodacom Foundation.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »