NAPE AKUTANA NA MAMA SAMIA LINDI

September 13, 2015

7
Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassani akimsalimia Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye alipowasili mpakani mwa mkoa wa Pwani na Lindi wakti akiwasili wilaya ya Kilwa mkoani Lindi, Septemba 12, 2015. Nape pia ni Mgombea wa Ubunge jimbo la Mtama mkoani Lindi.
8
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akijadiliana jambo ma Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hasaan alipowasili kufanya mkutano wa kampeni jimbo la Kilwa Kaskazini Septemba 12, 2015. Nape pia ni Mgombea wa Ubunge jimbo la Mtama mkoa wa Lindi.
1
Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mgombea Ubunge jimbo la Rufiji Mohammed Mchengerwa wakati wa mkutan wa kampeni uliofanyika Sepemba 12, 2015 katika jimbo hilo.
2
Aliyekuwa mgombea Ubunge jimbo la Rufiji Dk. Seleman Rashid akiteta jambo na aliyekuwa mgombea Ubunge jimbo la Mkuranga Adam Malima, wakati wa mkutano wa kampeni uliofanywa na Mama Samia katika jimbo la Rufiji septemba 12, 2015.
6
Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akihutubia mkutano wa kampeni uliofanyika Septemba 12, 2015, Ikwiriri, Rufiji mkoa wa Pwani.
4
Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akionyesha kadi za CUF na Chadema, alizopokea kutoka kwa wanachama wa vyama hivyo waliohamia CCM katika mkutano wa kampeni uliofanyika Ikwiriri, Rufiji mkoa wa Pwani, Septemba 12, 2015.
3 
Bibi Mwanahawa Saidi akitangaza kuhama CUF kurejea CCM, wakati wa mkutano wa kampeni wa Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan uliofanyika septemba 12, 2015, Ikwiriri Rufiji mkoawa Pwani.
5  
Maelfu ya wananchi wakiwa wamefurika katika mkutano wa kampeni wa CCM, uliofanyika septemba 12, 2015, Ikwiriri, Rufiji mkoa wa Pwani.
(Picha zote na Bashir Nkoromo)

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »