MGOSI: YANGA HAATUUMIZI KICHWA, NGOJA TUMALIZANE NA KAGERA SUGAR KWANZA

September 18, 2015

Nahodha wa Simba SC, Mussa Hassan Mgosi amesema akili zao kwa sasa zinaifikiria Kagera Sugar 

MECHI ZIJAZO LIGI KUU YA VODACOM TZ BARA

Septemba 19, 2015
Stand United Vs African Sports
Mgambo Shooting Vs Majimaji FC
Prisons Vs Mbeya City
Yanga SC Vs JKT Ruvu
Septemba 20, 2015
Mwadui FC Vs Azam FC
Mtibwa Sugar Vs Ndanda FC
Simba SC Vs Kagera Sugar
Coastal Union Vs Toto Africans
Septemba 26, 2015
Simba SC Vs Yanga SC
Coastal Union Vs Mwadui FC
Prisons Vs Mgambo Shooting
JKT Ruvu Vs Stand United
Mtibwa Sugar Vs Majimaji FC
Kagera Sugar Vs Toto Africans
Septemba 27, 2015
African Sports Vs Ndanda FC
Azam FC Vs Mbeya City
Na Princess Asia, DAR ES SALAAM
NAHODHA wa Simba SC, Mussa Hassan Mgosi amesema kwamba akili zao zipo kwenye mechi yao ya Jumapili dhidi ya Kagera Sugar na hawaumizwi kichwa hata dogo na mahasimu wao, Yanga SC.
Akizungumza na BIN ZUBEIRY juzi mjini Tanga, Mgosi amesema baada ya kushinda mechi mbili za mwanzo za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara sasa wanaelekeza nguvu zao katika mchezo wa tatu dhidi ya Kagera.
“Sioni sababu ya kuwazungumzia Yanga kwa sasa wakati mechi ijayo tunacheza na Kagera. Kwanza nataka nikuambie, hao Yanga hawatuumizi kichwa kabisa,”amesema.
Mgosi amesema kwamba wachezaji wote wa Simba SC kwa sasa akili yao inafikiria namna gani wataifunga Kagera Sugar ili kufikisha pointi tisa ndani ya mechi tatu.
Simba SC imeanza vyema Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada ya kushinda mechi zake zote mbili za mwanzo Uwanja wa Mkwakwani, Tanga 1-0 dhidi ya African Sports na 2-0 dhidi ya JKT Mgambo.
Sasa Wekundi hao wa Msimbazi walio chini ya kocha Muingereza, Dylan Kerr watacheza mechi yao kwanza nyumbani mwishoni mwa wiki, dhidi ya Kagera Sugar Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »