COASTAL UNION YAIPIGIA HESABU MWADUI

September 23, 2015
KOCHA Mkuu wa timu ya Coastal Union, Jackson Mayanja ameanza kikiandaa kikamili kikosi chake kwa ajili ya kuhakikisha kinaubuka na ushindi dhidi ya Mwadui FC kwenye mechi ya Ligi kuu soka Tanzania bara itakayochezwa wikiendi hii kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani.

Akizungumza , Mayanja alisema kuwa mapungufu yaliyojitokeza kwenye kikosi hicho kwenye michezo yao miwili tayari walikwisha kuyafanyia kazi kwa asilimia kubwa hivyo wapo vizuri kupambana kwa mafanikio.

Alisema kuwa tatizo ambalo linaisumbua timu hiyo la umaliziaji alikwisha kulifanyia kazi pamoja na lile la wachezaji kutokuwa makini hali inayomfanya kuanza kupata matumaini mapya ya kikosi hicho kurejesha makali yake.

Aidha alisema kuwa makosa madogo madogo yaliyoanza kuonekana kwenye mechi yao dhidi ya Toto African alikwisha kuyarekebisha baada ya kumalizika kwa mchezo huo ambao ulimalizika kwa timu hizo kutoka suluhu pacha ya kutokufunga.
 
“Nimekwisha kurekebisha baadhi ya mapungufu na sasa bado tunaendelea kujiandaa na michezo yetu inayokuwa ikiwemo ule wa Mwadui FC lengo kubwa likiwa kuhakikisha tunarudisha makali ya kikosi hiki “Alisema Kocha Mayanja.

Hata hivyo alisema kuwa dhamira yao bado ipo pale pale kuhakikisha wanafanya vizuri katika michuano ya Ligi kuu soka Tanzania bara msimu huu ili kuweza kupata nafasi ya kushiriki mashindano ya klabu bingwa afrika.


Coastal Union mpaka sasa imekwisha kucheza michezo mitatu ikipoteza miwili kwa kufungwa na Yanga na Ndanda ikiwemo kutoa sare ya bila kufungana ikiwa na pointi moja kwa michezo hiyo iliyokwisha kuchezwa.


















Share this

Related Posts

Previous
Next Post »