Mgeni Rasmi katika ufunguzi wa
maadhimisho ya wiki ya mazingira duniani Mheshimiwa Samuel Sitta
(aliyemuwakilisha Makamu wa Rais) akitia saini katika kitabu cha wageni
maa baadaya kuwasili katika bandala Ofisi ya Makamu wa Rais
wanaoshuhudia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais-Mazingira Mh.
Dkt Binilith Mahenge na Waziri wa Nchi Ofis ya Makamu waRais-Muungano
Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan. Ufunguzi huo ulifanyika katika viwanja
vya Tangamano katika jiji la Tanga.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa
Rais Dkt. Binilith Mahenge akimkaribisha mgeni Rasmi ili aweze kuzindua
maadhimisho ya wiki ya Mazingira duniani katika viwanja vya Tangamano
jijini Tanga.
Mkurugenzi wa Mazingira katika
Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Julius Ningu akitoa maelezo kwa mgeni Rasmi
Mheshimiwa Samuel Sitta alipotembelea banda la Ofisi ya Makamu wa Rais
katika maadhimisho ya wiki ya siku ya mazingira jijini Tanga. Wengine
wanaosikiliza ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais-Mazingira Mh.
Dkt Binilith Mahenge (kulia) na Waziri wa Nchi Ofis ya Makamu wa
Rais-Muungano Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan (kulia).
………………………………………..
Watanzana wametakiwa kutunza na
kuthamini mazingira kwa sababu ni urithi wa thamani kubwa sana kwa
kizazi cha sasa na kijacho. Hayo yamesemwa na Mgeni Rasmi katika
ufunguzi wa maadhimisho ya wiki ya siku ya mazingira Duniani, Mheshimiwa
Samuel Sita- Waziri wa Uchukuzi ambaye alimuwakilisha Makamu wa Rais
Mhe. Mohammed Gharib Bilal.
Akiongea na Wananchi katika viwanja vya Tangamano vilivyopo
katika jiji la Tanga Mheshimiwa Sita amesisitiza juhudi zaidi katika
suala zima la utunzaji wa mazingira na kuwaomba Wazazi kuelemisha watoto
wao umuhimu wa kuthamini mazingira. Aidha amewapa hongera Wananchi na
Viongozi wa jiji la Tanga kwa kutilia mkazo usafi wa mazingira na
kufanya jiji hilo kuibuka mshindi wa tatu katika mashindano ya usafi wa
mazingira kitaifa.
Akimkaribisha Mgeni Rasmi ili kufungua sherehe hizo Waziri wa
Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais-Mazingira Dkt. Binilith Mahenge aliesma ni
jukumu la kila mmoja kutunza na kuhifadhi mazingira hivyo basi kila
Mwananchi ajitahidi katika hilo.
Siku ya mazingira duniani hufanyika kila tarehe tano ya mwezi
Juni kila mwaka. Kauli mbiu ya mwaka huu ni Ndoto bilioni saba, dunia
Moja , tumia Rasilimali kwa uangalifu. Hii ikimaanisha kutumia vema
rasilimali zetu ili kutunza vema mazingira yetu.