NHIF YAENDESHA ZOEZI LA UPIMAJI WA AFYA JIJINI TANGA

June 02, 2015

1 
Luiza Mtafi wa NHIF akimpima mapigo ya moyo mmoja wa wananchama waliotembelea banda la Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya katika maonyesho ya tatu ya biashara ya kimataifa yanayofanyika katika viwanja vya Mwahako mjini Tanga.
2 
Afisa Matekelezo wa NHIF Bi. Shazy Amasha akitoa elimu kuhusu bima ya Afya  kwa watoto waliotembelea  banda la Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya katika maonyesho ya tatu ya biashara ya kimataifa yanayofanyika katika viwanja vya Mwahako mjini Tanga.
3 
Nesi Anna Jengo wa hospitali ya Bombo akimpima kiwango cha sukari Bw. Ahmed Ismail aliyetembelea katika banda la Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya kupata huduma hiyo.
4 5 
imu ya Maafisa wa NHIF ikifurahia ushindi baada ya kushinda nafasi ya kwanza katika kada ya afya kwenye maonyesho ya tatu ya biashara ya kimataifa yanayofanyika katika viwanja vya Mwahako mjini Tanga.
…………………………………………………………………………………
Na Catherine Kameka
Mamia ya wananchi wa Mkoa wa Tanga, wameendelea kujitokeza kwa wingi katika banda la Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) ili kupima afya zao.
NHIF Mkoa wa Tanga kwa kushirikiana na Makao makuu, inaendesha zoezi la upimaji afya bure kwa wananchi wa Tanga na maeneo ya karibu ikiwa ni sehemu ya majukumu yake ya kutoa huduma kwa wananchama wake  na wananchi kwa ujumla.
“Lengo kubwa la NHIF ni kuelimisha wananchama na jamii kuhusiana na magonjwa yasiyoambukiza  ambayo yamekuwa yakiongezeka kwa kasi”
Meneja wa NHIF Tanga Bw. Ali Mwakababu aliyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika banda la Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya lililopo katika viwanja vya Mwahako ambapo maonyesho ya tatu ya biashara ya kimataifa yanafanyika.
Aliongeza kwa kusema kuwa katika zoezi hili wanachama na wananchi wa mkoa wa Tanga watapimwa shinikizo la damu (BP), sukari na uzito na urefu na kuainisha uwiano kati ya uzito na urefu na watakaokutwa na matatizo watapata ushauri wakitaalamu na madaktari wa Mfuko waliopo kwenye banda hilo.
Hivyo alitumia fursa hiyo kuwaomba wakazi  wa Tanga kuutumia muda huo kwa kujitokeza katika viwanja vya Mwahako ili kupima afya zao.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »