Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) yaandaa utaratibu wananchi kuandikishwa kwenye daftari la kudumu la wapiga kura

June 02, 2015

images 
Na Masanja Mabula -Pemba
………………………………………
Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) Jecha Salim Jecha amesema kuwa hakuna mwananchi aliyetimiza sifa na masharti ambaye atakosa fursa ya kuandikishwa kwenye daftari la kudumu la wapiga kura ambalo limeanza katika Wilaya ya Micheweni Pemba .
Amesema kuwa Tume imendaa utaratibu ambao utawafanya wananchi wote waliotimiza mashari na wenye vitambulisho vya Mzanzibar Mkaazi ambao hawajawahi kuandikisha kwenye daftari kuandikishwa kwenye daftari hilo .
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi wakati wa zoezi hilo Wilayani hapa , Jecha ametumia fursa hiyo kuwataka wananchi waliotimiza umri wa miaka kumi na nane na ambao hawakuandikisha kwenye daftari kufika vituoni kwa ajili ya kuandikishwa .
Amefahamisha kwamba kujiandikisha katika daftari ni kutumia haki ya msingi kidemokrasia na kikatiba hivyo ni vyema kila mmoja kuitumia haki hiyo ambayo itamwezesha kupata fursa ya kumchagua kiongozi anayemtaka katika uchaguzi Mkuu baadaye mwaka huu .
“Tume tumejipanga vyema kwamba na kwamba hakuna mwananchi ambaye atakosa haki yake ya kuandikishwa ambaye ametimiza masharti na vigezo , hivyo nawaomba wananchi wajitokeze kwenye vituo vya kuandikisha ” alisema .
Aliongeza kwamba “Hii ni haki ya kila kwa mujibu wa sheria na katiba kwani ndiyo inayompa fursa ya kuweza kuchagua kiongozi anayemtaka na kwamba nawaomba sana waitumie fursa hii ” alisisitiza Jecha .
Nao baadhi ya wananchi waliozungumza na mwandishi wa habari hizi wameipongeza tume ya Uchaguzi kutokana na maandalizi iliyoyafanya kwani hakuna mwananchi ambaye amelalamikia utaratibu huo .
“Utaratibu huu ni lazima Tume tuipongeze kwani ni mzuri hakuna fujo , watendaji wake wako makini cha msingi kila mwananchi mwenye sifa afike kuandikishwa katika daftari ” alisema Raya Ali wa Micheweni .
Kwa upande wake Katibu wa CCM Mkoa wa Kaskazini Pemba Khadija Nassor Abdi amewataka wanasiasa kuacha kutoa vitisho kwa wananchi wenye asili ya Tanzania Bara ambao wanataka kuwazuia ili wasijiandikishe katika daftari licha kwamba wametimiza masharti na vigezo vyote .
“Tumebaini kuwepo na njama zinazofanywa na wapinzani kwa kutaka kuwazuia ndugu zetu wenye asili ya Bara hata kama wametimiza masharti  , wanatishwa lakini sisi tumeibaini na tunatoa wito kwa wanasiasa kuacha kupata uhuru ili watumie haki yake kikatiba ” alieleza Khadija .
Awali Mbunge wa Jimbo la Konde (CUF) Khatib Said aliwataka mawakala wa Chama hicho kuwawekea pingamizi baadhi ya vijana wenye asili ya Bara akidai kwamba hawajatimiza masharti ikiwemo umri wao .

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »