Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiifungua Semina ya
siku moja ya Usafiri Barabarani kwa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi
iliyofanyika kwenye ukumbi wa juu wa Baraza la Wawakilishi Mbweni.
Waziri
wa Miundombinu na Mawasiliano Zanzibar Mh. Juma Duni Haji akitoa
maelezo kwenye Semina ya Usafiri wa Barabarani kwa Wajumbe wa Baraza la
Wawakilishi kabla ya ufunguzi wa Senmina hiyo.
Wajumbe
wa Baraza la Wawakilishi pamoja na wadau wa usafiri walioshioriki
semina ya usafiri wa bara barani wakifuatilia Horuba ya Mgeni rasmi
Balozi Seif hayupa Pichani.
Mkurugenzi
wa Idara ya Usafiri na Leseni Nd. Suleiman Kirobo akitoa Mada kwenye
Semina ya Usafiri wa Barabarani iliyoshirikisha wajumbe wa Baraza la
Wawakilishi pamoja na wadau wa sekta ya usafiri.
Mkuu
wa Kikosi cha UsalamaBara barani Kamishna Msaidizi wa Polisi { ACP }
Nassor Ali Moh’d akitoa ufafanuzi wa ajali za barabarani zinazoonekana
kuongezeka kutokana na matumizi mabovu ya bara bara kwenye semina ya
usafiri wa bara barani.
Picha na – OMPR – ZNZ.
Viongozi
wenye fursa za maamuzi pamoja na nyadhifa katika Taasisi za Umma Nchini
wameombwa kuwaelimisha Vijana wao wanaoendesha vyombo vya moto kufuata
sheria za usalama barabarani badala ya kuwasubiri kuwaombea
wanapokamatwa na askari wa usalama bara barani kwa kufanya makosa
tofauti ambayo mengi kati yao ni yale ya makusudi.
Akiifunguwa
Semina ya usafiri wa Barabarani kwa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi
hapo kwenye ukumbi wa Baraza hilo Mbweni Makamu wa Pili wa Rais wa
Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisema tabia ya baadhi ya viongozi
kuwaombea Vijana wao kuwachiliwa kwa makosa yao ya makusudi ni kuwavunja
moyo Polisi na kupelekea kuonekana hawatekelezi majukumu yao ipasavyo.
Balozi
Seif alisema imekuwa ni jambo la kawaida hivi sasa kwa baadhi ya
Viongozi kuwaombea vijana wao wasifikishwe Mahakamani wakati
wanapofanya makosa jambo ambalo kwa kiasi kikubwa linaondosha heshima
yao ndani ya jamii.
Alisema
uvunjwaji wa sheria za usafiri wa barabarani unaofanywa na watumiaji wa
barabara hizo kama waendesha vyombo vya moto, gari zinazobururwa na
wanyama, baskeli na ha waendao kwa miguu husababisha ajali zinazoleta
madhara kwa Taifa.
Alisema
jamii imekuwa shahidi iliwaona Vijana wanaoendesha Vyombo vya ringi
mbili Vespa na Pili pili wakipakizana watu zaidi ya wawili katika chombo
huku wakifukuzana kwa mwendo wa kasi wakiwa wamekaa katika mkao wao
maarufu { T. ONE } huku vyombo hivyo vikichomolewa breki kwa makusudi.
Alisema
chakusikitisha zaidi baadhi ya vijana hao huendesha vyombo hivyo kwa
ringi moja tuu vikiwa kwenye mwendo mkali bila ya hata kuvaa kofia ngumu
lakini jambo la ajabu zaidi baadhi yao ni viongozi katika Jamii hii.
Mapema
Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano Mh. Juma Duni Haji alisisitiza
umuhimu wa mashirikiano ya pamoja kwa Taasisi zote zinazosimamia
shughuli na harakati za Bara bara ndio njia pekee itakayosaidia
kupunguza au kuondosha kabisa changamoto ya usafiri wa Barabarani.
Wakitoa
mada kwenye semina hiyo ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kuhusu
usafiri na usalama Barabarani Mkurugenzi wa Idara ya usafiri na Leseni
Nd. Suleiman Kirobo, Mkuu wa Kikosi cha usalama Barabarani Msaidizi
Kamishna wa Polisi ACP Nassor Ali Moh’d pamoja na Mdau wa Sekta ya
Usafiri Bwana Waziri Hashim walisema zipo sheria zilizopitwa na wakati
mabazo kutofanyiwa marekebisho ya haraka zitaendelea kuchangia matatizo
yanayopatikana katika matumizi ya usafiri wa Bara barani.
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
6/6/2015.