Na Masanja Mabula,Pemba.
MKUU wa Mkoa wa kaskazini pemba Mhe Omar Khamis Othman amelitaka Shirika la Bandari Zanzibar kuharakisha ukarabati wa bandari ya wete ili
kudhibiti ongezeko na bandari bubu katika Mkoa huo .
Amesema
kuwa ongezeka la Bandari bubu katika mkoa huo inasababishwa na
kutokuwepo kwa chombo cha uhakikisha cha usafiri kutoka Pemba -Tanga ,
hali ambayo inawafanya wananhi kutumia vyombo na bandari zisizo rasmi .
Kauli hiyo ameitoa huko ofisini kwake wakati akizungumza na ujembe
kutoka Shirika la bandari zanzibar ukiongozwa na mkurugenzi wa shirika
hilo Abdalla Juma Abdalla .
mkuu
huyo wa mkoa pia ametumia fursa kulitaka shirika la bandari zanzibar
kuandaa utaratibu mzuri wa uondokaji na uingiaji wa abira katika bandari
ya wete ili kudhibiti upitishwaji wa madawa ya kulevya .
Naye
mkurugenzi wa shirika la bandari zanzibar bw abdalla juma abdalla
amesema kuwa shirika limepanga kuifanyia matengenezo bandari ya wete
katika kipindi cha bajati ijayo .
Amesema kuwa kukamilika kwa matengenezo hayo yataondoa usumbufu wanaoupata abira wanaosafiri kutoka Pemba kwenda Tanga .
Hata
hivyo mkurugenzi huyo amekiri kuwa hali ni ngumu kuweza kudhibiti
bandari bubu kutokana na tatizo la ukosefu wachombo cha uhakikisha
wanachotumia abiria kusafiri na kusafirishia mazao .