AFRICAN SPORTS WAPITISHA KATIBA YAO,SASA WAPO KAMILI KWA USAJILI

May 12, 2015
WANACHAMA arobaini na tisa waliohudhuria mkutano wa klabu hiyo kati ya sabini na sita wa klabu ya African Sports juzi walipitisha katiba mpya wa klabu hiyo ambayo itawapa dira kuu ya kuelekea ushiriki wao katika Michuano ya Ligi kuu soka Tanzania bara .

Katiba hiyo inaendana na katiba nyengine ya vilabu vinavyoshiriki ligi kuu ikiwemo ile ya shirikisho la soka hapa nchini ambapo ilipitishwa na wanachama hao kwenye mkutano wa wanachama wa klabu hiyo ambao ulifanyika kwenye ukumbi wa Splended jijini Tanga.

Akizungumza mara baada ya kuipitisha katiba hiyo, Mwenyekiti wa Klabu ya African Sports, Hassani Shehe alisema kuwa wanamshukuru mungu kupitisha katiba hiyo ambayo ilikuwa ni muhimili mkubwa kwa maendeleo ya timu yao baada ya kupanda daraja ya Ligi kuu.

Hassani alisema kuwa mkutano huo ulikuwa na mambo muhimu mawili ambapo la kwanza lilikuwa ni kupitisha katiba hiyo ikiwemo kukutana na wanachama kwa ajili ya kutambuana.

Alisema kuwa baada ya kumalizika suala hilo muhimu kwao watajiandaa na taratibu wa uchaguzi mkuu wa viongozi ambao wataiongoza klabu hiyo na usajili kwa ajili ya msimu mpya wa Ligi kuu hapa nchini.

Awali akizungumza katika mkutano huo,Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Tanga(TRFA),Salim Omari aliwataka viongozi na wanachama wa klabu hiyo kuhakikisha wanashikamana ili kurudisha makali ya timu hiyo ya miaka ya nyuma.

      “Tunafahamu vizuri enzi za miaka ya nyuma timu hii ilipokuwa ikifanya mambo makubwa katika michuano ya Ligi kuu hivyo viongozi hakikisheni hili linajirudia msimu ujao lakini kikubwa kuweni na ushirikiano “Alisema Salim.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »