WAKULIMA ZALISHENI BIDHAA ZENYE UBORA

March 01, 2015

index
Mahmoud Ahmad Arusha
…………………………………………………
Wajasiriamali na wakulima hapa nchini wametakiwa kuhakikisha wanazalisha bidhaa zenye ubora zitakazofaa kwenye masoko ya uhakiki sanjari na kuweza kuyamudu masoko kwani hilo limekuwa ndio tatizo la wajasiriamali wengi kutoweza kuandaa bidhaa kwa ubora.
Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Chuo cha Veta Mkoani hapa Banga Deusdedit wakati akifunga maonyesho ya wauzaji wa bidhaa za kilimo na mikopo yaliofanyika kwa siku tatu jijini hapa na kumalizoika mwishoni mwa wiki.
Banga alisema kuwa malengo ya maonyesho hayo ya EFTA na dhamira yao iwe chacu kwa wajasiriamali ambao wamepata mafunzo mbalimbali ya kuweza kujiajiri na kuweza kuzalisha bidhaa zenye ubora na uhakika kwenye masoko ya ndani na nje.
Aliongeza kuwa unapukuwa na soko la uhakika na bidhaa zenye viwango vyenye ubora huhitaji kutumia nguvu kuitangaza kwani kuna msemo wa Kiswahili kibaya kinajitembeza kizuri kinajiuza hivyo mzalishe bidhaa zenye ubora zitakazopata soko la uhakika.
“Mara nyingi nimekuwa nikangalia maonyesho mbalimbali ya wajasiriamali na wamekuwa wakionyesha bidhaa mbalimbali wanazozalisha lakini hazipo kwenye masoko ya uhakika ni wajibu wenu mkatumie mafunzo haya mliopata kuhakikisha mnayasogelea masoko ya uhakika”aliongeza Banga.
Mmoja wa washiriki wa maonyesho hayo kutoka Tanzania Farmers Service Center Faustine Urio aliwataka watanzania kuhakikisha wanazalisha bidhaa zenye ubora wa uhakika na kuhakikisha wanauwezo wa kuhudumia masoko yao kwa uhakika bila ya kukatisha bidhaa kwenye masoko.
Urio alisema kuwa kampuni yao imejipanga kuhakikisha wanawalitea watanzania bidhaa na vifaa vyenye viwango vya kisasa vitavyowasaidia kuzalisha na kutengenea bidhaa zenye ubora na kuhakikisha Maendeleo kwa watu wa kada hiyo yanapatika kwa uhakika.
 
“TFSC kama mlivyoona tulikuwa tunaonyesha na kukopesha aina m,bali mbali za matrekta na vifaa vya kilimo vitakavyowasaidia wakulima na wajasiriamali kuweza kufikia malengo waliojiwekea na washauri mtumie bidhaa zetu”alisema Urio.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »