Moto umeibuka katika hostel za chuo cha UDSM zilizoko Mabibo (Mabibo
hostel) na bado unaendelea hadi sasa ila chanzo hakijajulikana.
Waziri Mkuu wa Serikali ya wanafunzi wa chuo hicho cha UDSM Bwana Gibson
George amesema kuwa chanzo hakijajulikana na nini ila moto umesambaa
maeneo mbalimbali ya hosteli hizo.
"Watu wa zimamoto tumewapigia mapema sana ila wamechelewa kufika hadi
muda huu ndio wamefika, tumejaribu kuuzima moto na umepungua kidogo japo
bado unaendelea kwa baadhi ya vyumba" alisema Waziri Mkuu huyo
Imeripotiwa muda mfupi uliopita kuhusu tukio la moto katika Hostel za Mabibo ambapo wanaishi wanafunzi wa Chuo Kikuu Dar es Salaam.
Taarifa za awali zinasema kuwa chanzo cha moto huo ni shoti ya umeme, hakuna taarifa ya mtu yoyote kuathirika na moto huo mpaka sasa.
Naendelea kufuatilia tukio hili, nitakufikishia taarifa yote muda wowote kuanzia sasa pamoja na picha zaidi.
Hautopitwa na stori yoyote inayonifikia , niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia www.tangakumekucha.blogspot.com
Imeripotiwa muda mfupi uliopita kuhusu tukio la moto katika Hostel za Mabibo ambapo wanaishi wanafunzi wa Chuo Kikuu Dar es Salaam.
Taarifa za awali zinasema kuwa chanzo cha moto huo ni shoti ya umeme, hakuna taarifa ya mtu yoyote kuathirika na moto huo mpaka sasa.
Naendelea kufuatilia tukio hili, nitakufikishia taarifa yote muda wowote kuanzia sasa pamoja na picha zaidi.
Hautopitwa na stori yoyote inayonifikia , niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia www.tangakumekucha.blogspot.com