Mkurugenzi
wa Masoko wa kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania, Levi
Nyakundi (kushoto) na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa kampuni hiyo,
Beatrice Singano Mallya (kulia) wakionyesha kipeperushi wakati
wakizindua rasmi promosheni ya 'Airtel Yatosha Zaidi' ambapowateja
watakaojiunga na bando la yatosha watapata nafasi ya kushinda kila siku
gari moja aina ya Toyota IST. Uzinduzi wa promosheni hiyoulifanyika
jijini Dar es Salaam jana.
Mkurugenzi
wa Masoko wa kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania, Levi
Nyakundi (kulia) na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa kampuni hiyo, Beatrice
Singano Mallya (kushoto) wakionyesha baadhi magari yatakayoshindaniwa
wakizindua rasmi promosheni ya 'Airtel Yatosha Zaidi' ambapo wateja
watakaojiunga na bando la yatosha watapata nafasi ya kujishindia kila
siku gari moja aina ya Toyota IST. Uzinduzi wa promosheni hiyo
ulifanyika jijini Dar es Salaam jana.
Mwendesha
pikipiki akinyesha umahiri wake kunogesha wa uzinduzi wa promosheni ya
'Airtel Yatosha Zaidi' ambapo wateja watakaojiunga na bando la yatosha
watapata nafasi ya kujishindia kila siku gari moja aina ya Toyota IST.
Uzinduzi wa promosheni hiyo ulifanyika jijini Dar es Salaam jana.
********
Airtel
Tanzania leo imezindua promosheni kabambe ijulikanayo kama Airtel
Yatosha Zaidi kwa wateja wanaotumia vifurushi vya AirtelYatosha kuweza
kujishindia gari Aina ya Toyota IST kila siku
Akiongea
wakati wa uzinduzi wa promosheni hiyo Mkurugenzi wa Masoko ya Airtel
Bwana Levi Nyakundi alisema” promosheni hii ni nafasi ya peeke wa wateja
wetu wanaojiunga na vifurshi vya Airtel yatosha vya siku, wiki na mwezi
kupata faida zaidi kutokana pesa wanazozitumia. Nia yetu kuhakikisha
tunatoa huduma na bidhaa bora kwa kupitia huduma yetu ya Airtel Yatosha
huku tukiwazawadia wateja wetu zawadi nono.
Tunaamini
promosheni hii itawapatia wateja wetu uzoefu tofauti wakati wote
wakitumia huduma zetu za Airtel Yatosha. Zaidi ya wateja wetu
kijishindia magari promosheni hii ya Airtel Yatosha Zaidi itawapatia
wateja wetu vifurushi zaidi “Aliongeza Nyakundi
Akiongea
kuhusu namna ya kushiriki Mkurugenzi wa mawasiliano wa Airtel Bi
Beatrice Singano Mallya alisema” ili kushiriki kwenye promosheni hii
wateja wanatakiwa kuendelea kununua vifurushi vyao vya Yatosha vya siku,
wiki na mwenzi. hakuna gharama ya ziada, kwa kununua vifurushi vya
yatosha tayari utakuwa umeunganishwa kwenye droo ya yatosha zaidi na
kupata nafasi ya kujishinidia Toyota IST moja kila siku.
Hii
ni promosheni ya aina yake ambapo wateja wetu wanazawadiwa kutokana na
matumizi yao ya kawaida ya vifurushi vya Yatosha. tunatoa wito kwa wale
ambao hawajajiunga na vifurushi vya Airtel yatosha kufanya hivi na
kupata nafasi ya kushinda gari moja kila siku”aliongeza Mallya
Kununua
vifurushi vya yatosha wateja wanaweza au kupiga *149*99#, kunua kwa
kupitia huduma ya Airtel Money au kwa kununua vocha ya Airtel yatosha
inayopatikana katika maduka yetu nchi nzima.
Mwaka
Jana Airtel ilizindua huduma ya kisasa ya kibunifu na yenye vifurushi
vya gharama nafuu sokoni. Kuzinduliwa kwa promosheni hii ya Airtel
yatosha Zaidi ni mwendelezo wa dhamira ya Airtel ya kutoa huduma bora
huku ikiwazawadia wateja wake kwa kutumia huduma zake.