Aliyekuwa
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo leo amekabidhi
Ofisi kwa Waziri mpya wa wizara hiyo George Simbachawene.
Katika
makabidhiano hayo, Prof Muhongo ameonya juu ya matumizi mabaya ya Ofisi
yanayoambata na rushwa ili kuwasaidia watanzania masikini wanaoitegemea
sekta hiyo kwa maendeleo ya uchumi wao.
Muhongo
amemuasa Simbachawene juu ya umakini na kufanya kazi kwa kuzingatia
mikataba inayoweza kuwanuifaisha watanzania na rasilimali zao.
Amemsifu
Simbachawene kuwa hakuahi kuonesha ubinafsi wala tamaa na muda wote
alikuwa akizungumzia juu ya kuwatumikia watanzania alipokuwa naibu
waziri wa wizara hiyo, kwahiyo ana imani naye.
Amesema
Tanzania ni lazima ilenge katika kujenga uchumi imara kupitia sekta ya
Nishati na Madini inayokua kwa kasi ili watanzania pia waweze kukua
kiuchumi.
Kwa
upande wake Simbachawene amesema ataendeleza mazuri yaliyoachwa na
mtangulizi wake kwa kuweka uwazi kwa kila kitu kinachofanyika, kwani
ofisi ya umma sio mali ya mtu.