SERIKALI IMETENGA BILION 2.8 KUKAMILISH MIRADI YA MAJI VIJIJI KUMI KATA YA KWEDIBOMA WILAYANI KILINDI.

July 13, 2014
Rais Jakaya Kikwete akifungua bomba la maji mara
baada ya kuzindua mradi wa maji  kijiji cha Kwediboma kata ya
Kwediboma wilayani Kilindi Mkoani Tanga wenye thamani ya shilingi
milioni 571,361,391 ambapo mpaka kufikia hatua hiyo ya kuzinduliwa
ulikuwa umegharimu kiasi cha sh.milioni 316,197,327, Rais Kikwete yupo
mkoani Tanga katika ziara ya kikazi ya siku tano aliyoanzia wilaya ya
Kilindi
KILINDI.
KATIKA kukabiliana na tatizo la maji katika kata ya Kwediboma iliyopo  wilayani Kilindi serikali imetenga kiasi cha sh. Bilion 2.8 kwa ajili ya kukamilisha mradi wa maji safi kwenye vijiji kumi vinavyounda kata hiyo.

Rais Kikwete amebainisha hayo jana wakati akihutubia wananchi wa kata
  ya Kwediboma kabla ya kuzindua ujenzi wa mradi wa Maji ya Bomba wa kijiji cha Kwediboma unatekelezwa kupitia mpango wa kuendeleza sekta ya maji kwa ufadhili wa Benki ya Dunia kwa kushirikiana na serikali ya Tanzania.

Alisema fedha hizo zimetengwa katika bajeti ya mwaka wa fedha ujao wa
  2014/2015 ili kusaidia kupunguza ukubwa wa tatzio la upatikanaji wa huduma hiyo kwa wananchi hasa waishio maeneo ya vijijini.

"Ndugu zangu pamoja na serikali kuwekeza fedha hizi tambueni kwamba
  kama jamii mnalo jukumu kubwa la kuhakikisha mradi huu unatunzwa ili uwe endelevu kwa ajili ya kutoa huduma kwenu na vizazi vijavyo...naomba wananchi waote washiriki kutimiza jukumu hili ili kutoa huduma endelevu", alisema rais.

Vijiji vitakavyonufaika na huduma ya maji kupitia fedha hizo ni

Mpalahala, Kwedigole,Kileguru,Mzinga ambavyo kwa sasa havina huduma ya maji hasa baada ya ya chanzo chao tegemezi ambacho kilikuwa ni Malambo mawili yaliyojengwa na halmashauri kupitia mradi wa DADPS kubomolewa na mvua msimu uliopita.
Rais Jakaya Kikwete kushoto akimtwisha ndoo ya maji
mkazi wa kijiji cha Kwediboma kata ya Kwediboma wilayani Kilindi
Mkoani Tanga mara baada ya kuzindua mradi wa maji ya bomba kwenye
kijiji hicho wenye thamani ya kiasi cha sh.milioni 571,361,391 ambapo
mpaka kufikia hatua ya uzinduzi huo zilikuwa zimekwisha kutumika kiasi
cha sh.milioni 316,197,327,Rais Kikwete yupo mkoani Tanga katika ziara
ya kikazi ya siku tano aliyoanzia wilaya ya Kilindi
Awali akisoma taarifa kuhusu mradi huo, Katibu wa Kamati ya Mradi huo
  Ibrahim Abdallah alisema hadi kukamilika kwake unatarajiwa kugharimu kiasi cha sh. 517,364,391 na kwamba mpaka sasa zimetumika sh. 316,197,327 kwa ajili ya kukamilisha kazi za awamu ya kwanza ya mradi.

""Mradi huu unaotarajiwa kunufaisha wakazi 7,139 wa kijiji cha

Kwediboma ulianza mwaka 2010 baada ya kuibuliwa na wananchi ....katika awamu ya pili iliyoanza mwaka 2013 tulijenga miundombinu pamoja na vituo 24 vya kusambazia maji kijijini, nyumba ya kuhifadhia mitambo ya kusukumia maji toka kwenye chanzo , tangi, kufunga dira", alisema.

Katibu huyo alisema kubomoka kwa malambo hayo tayari kulisababisha
  ugomvi mkubwa baina ya wakulima na wafugaji ambao wamekuwa wakihama hama kusaka malisho.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »