AKUDO IMPACT KUPAGAWISHA BONANZA LA SIKUKUU YA IDDI MOSI MSASANI BEACH CLUB KAWE

July 22, 2014
BENDI ya Akudo Impact  “Vijana wa Masauti”watafanya onyesho kali la Bonanza wakati wa sikukuu ya Iddi Mosi kwenye Ukumbi wa Msasani  Beach Club Kawe Dar es Salaam litakaloanza saa nane mchana hadi Majogoo

Akizungumza kwa njia ya simu na TANGA RAHA BLOG,Meneja wa Akudo Impact,Juma Abajalo
  alisema maandalizi ya kuelekea bonanza hilo lililopewa jina la Shangwe za sikukuu ya Iddi limekamilika kwa asilimia kubwa.

Abajalo alisema wapenzi wa mziki wa dansi hapa nchini wakae mkao wa
  kula wakisubiria burudani kabambe itakayotolewa na wasanii wanaounda bendi hiyo maarufa hapa nchini wakiwemo Taasisi Masela Zegrebu Butam,Alen Kabasele mtoto wa pepekale Dipron aliyekuwa malaika bendi na Rap Fadii.

Alisema baada ya kumalizika onyesho hilo la Msasani Beach bendi hiyo
  itaondoka usiku kuelekea Visiwani Zanzibar Iddi Pili na siku Ijumaa inayofuata watahamia kufanya onyesho lao katika ukumbi wa Hiltech Banana Ukonga na Jumamosi watafanya kwenye ukumbi wa Cheetozi Miti Mirefu Sayansi.

Aidha alisema budurani zote hizo zitakuwa ni za kiwango cha hali ya
  juu na kuwataka wapenzi wa mziki huo kujitokeza kwa wingi kushuhudia maonyesho hayo yatakayokuwa gumzo mara baada ya kumalizika mfungo mtukufu wa ramadhani.

Hata hivyo alisema katika kuhakikisha onyesho hilo warembo

watakaokonga nyoyo wapenzi watakaojitokeza wataongozwa na Mrembo Raisa ambaye amekuwa akifanya vizuri sana hasa anapokuwa stejini.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »