WAGOSI WA KAYA KUJA NA MWANAUME KUSHUGHULIKA SOON.

May 05, 2014
NA OSCAR ASSENGA, TANGA.
KUNDI la Mziki wa Bongo Fleva Mkoani Tanga la ‘Wagosi wa Kaya”linatarajiwa kuachia wimbo wake mpya hivi karibu utakaoitwa “Mwanaume Kushughulika” waliomshirikisha nguli za mziki wa Taarabu nchini Khadija Koppa.

Akizungumza na TANGA RAHA BLOG LEO mmoja wa wanasanii wanaounda kundi hilo,John Simba “Dr.John”alisema waliamua kuungana tena pamoja mara baada ya kufikia makubaliana ya kufanya kazi pamoja lakini watakuwa chini ya uangalizi kwa ajili ya kusimamia kazi zao za kundi hilo ili kusiwe na malalamishi ambayo yanaweza kujitokeza ndani yao.

Dr.John alisema wimbo huo utakuwa gumzo kutokana na kuwepo kwa vionjo mbalimbali hivyo kuwataka mashabiki wao kukaa mkao wa kula kwani wamepania kufanya mapinduzi kwenye mziki huo.

Alisema miongoni mwa nyimbo ambazo tiyari walishazitoa ni pamoja na "Tiza Uya Kaya"ambayo ina misemo ya kisambaa wenye maana tumerudi nyumbani wakiwa wameshirikisha Lady Jay Dee na Gahawa ambazo zinatarajiwa kufanya vizuri.

Akizungumzia mziki wa kizazi kipya hapa nchini maarufu kama bongofleva,Dr.John alisema kwa sasa unalipa sana hivyo kuwataka wasanii kuendelea kukaza buti kwa kutunga tungo zenye jumbe nzuri kwa jamii.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »