SUPER STAR DIAMOND PLATZNUM AAAHIDI KUTENDA HAKI KWA WANANCHI WA MTWARA ONA ALICHOSEMA LIVE!!

May 03, 2014

Mwanamuziki Mahiri wa muziki wa kizazi kipya nchini Diamond Platinum,akiwapagawisha mashabiki wake wa mkoa wa mtwara waliofurika katika Tamasha la Ties & Heels lililodhaminiwa na Vodacom Tanzania na kufanyika kwenye ukumbi wa Makonde beach Mkoani Mtwara jana.
Mwanamuziki Mahiri wa muziki wa kizazi kipya nchini Diamond Platinum,akicheza na madansa wake wakati wa  Tamasha la Ties & Heels lililodhaminiwa na Vodacom Tanzania na kufanyika kwenye ukumbi wa Makonde beach Mkoani Mtwara jana.
 
Mwanamuziki Mahiri wa muziki wa kizazi kipya hapa nchini Diamond Platinum ameahidi kuwatendea haki wakazi wa mikoa ya kusini kila mwaka kwa kile anachodai mafanikio makubwa ya ndoto yake ya kuwa mwanamuzi bora hapa nchini imeanzia mkoa wa Mtwara.
 
Mwanamuziki huyo  aliambatana na  kipenzi chake, Malkia wa Bongo Movie nchini, Wema Sepetu – ‘Beautiful Onyinye’ au Madame kama mashabiki wake walivyokuwa wakimuita amethibitisha kauli hiyo  kwa mashabiki wake waliofurika katika tamasha maalumu la Ties & Heels lililofanyika katika ukumbi wa makonde  beach Mkoani Mtwara na kudhaminiwa na kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania.
 
Amesema tangu kuanza kwake kujiingiza kuwa mwanamuzi wa muziki wa kizazi kipya alianza kwa shoo yake mkoani mtwara ambapo ilionyesha kuwakuna wapenzi wengi na aliendelea kujulikana maeneo mengi hapa nchini kutokana na wapenzi walivyoanza kukumkubali, na ndipo aliwaahidi wapenzi hao kuwa ataendelea kuwasili mkoani humo kila mwaka kwa kulipa fadhila kwa mafanikio anayoyapata.
 
Akizungumzia juu ya shoo hiyo iliyokuwa ya kukata na shoka kwa wakazi wa mkoa wa Mtwara, Mkuu wa Kanda ya kusini wa Vodacom Tanzania, Henry Tzamburakis amebainisha kuwa tukio hili limeandaliwa ikiwa ni sehemu ya burudani kwa wateja wetu, kufurahi kwa pamoja na kuwashukuru wateja wetu kwa kuendelea kutumia huduma zetu.
 
“Hakuna kitu ambacho tunajali na kukithamini kama wateja wetu, haijalishi wawe kona gani ya Tanzania, walipo popote tutawafikia. Vodacom imekuwepo nchini kwa zaidi ya miaka kumi sasa na kwa kipindi chote hicho watanzania wameonyesha kutuunga mkono na kutufanya tuwe mtandao unaaongoza kwa mawasiliano nchini.” Alisema Tzamburakis.
 
Kwa kuongezea Tzamburakis amewashukuru  wakazi na mashabiki wote wa Diamond na wapenzi wa muziki wa Bongo Flava kujitokeza kwa wingi kwani mbali na burudani wamenufaika na baadhi ya huduma na bidhaa mbali mbali za Vodacom.
 
Nae Malkia wa Bongo Movie nchini, Wema Sepetu alieambatana na mpenzi wake alisema hakuona shida kumsindikiza asali wake wa moyo mtwara yote haya kwaajili ya mashabiki wao. Kwa tafsiri nyingine mashabiki wa Mtwara wanabahati kubwa ya kutembelewa nasi na tutadumisha utamaduni huu kila mwaka.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »