Hosni Mubarak ahukumiwa miaka mitatu gerezani

May 21, 2014
Mahakama moja nchini Misri imemhukumu aliyekuwa rais wa nchi hiyo Hosni Mubarak kifungo cha miaka mitatu gerezani kwa mashitaka ya wizi wa fedha za umma pamoja na wanawe wawili wa kiume ambao wameshitakiwa kwa makosa hayo hayo kifungo cha miaka minne gerezani.

Watatu hao pia wametozwa faini ya  pauni milioni 21.1 za Misri na kuagizwa kurejesha pauni nyingine milioni 125 kwenye hazina ya taifa.

Washitakiwa wengine hawakutikana na hatia .Wakati huo huo mahakama nyingine nchini humo imewahukumu vifungo mbali mbali wanachama wa udugu wa kiislamu kwa mashitaka ya kuhusika katika ghasia zilizotokea katika jimbo la Nile Delta mwezi Agosti mwaka jana. 

45 kati yao wamehukumiwa kifungo cha maisha gerezani huku wengine wakipiwa vifungo vya kati ya miaka mitatu na kumi gerezani.
 Polisi walilazimika kutumia mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya waandamanaji waliokuwa nje ya mahakama hiyo.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »