Watatu hao pia wametozwa faini ya pauni milioni 21.1 za Misri na kuagizwa kurejesha pauni nyingine milioni 125 kwenye hazina ya taifa.
Washitakiwa wengine hawakutikana na hatia .Wakati huo huo mahakama nyingine nchini humo imewahukumu vifungo mbali mbali wanachama wa udugu wa kiislamu kwa mashitaka ya kuhusika katika ghasia zilizotokea katika jimbo la Nile Delta mwezi Agosti mwaka jana.
45 kati yao wamehukumiwa kifungo cha maisha gerezani huku wengine wakipiwa vifungo vya kati ya miaka mitatu na kumi gerezani.
Polisi walilazimika kutumia mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya waandamanaji waliokuwa nje ya mahakama hiyo.
EmoticonEmoticon