MMoja
ya wakulima wa Mahindi Wilaya ya Handeni mkoani Tanga Bw. Adalbertus
Bubelwa wa pili kutoka kushoto akimwelezea Mkuu wa wilaya ya handeni Bw.
Muhingo Rweyemamu, jinsi alivyoandaa shamba lake. Mkuu huyo wa wilaya
alikuwa katika ziara ya kuwatembelea wakulima katika vijiji mbalimbali
wilayani humo kuangalia mazao mashambani.
Mkuu
wa wilaya ya Handeni Bw. Muhingo Rweyemamu, kushoto ambaye ni mwenye
shamba akipata maelekezo kutoka kwa Afisa Kilimo wa Wilaya hiyo Bw.
Yibarik Chiza, aliyemtembelea Mkuu huyo wa wilaya shambani kwake
Afisa
Kilimo wa wilaya ya Handeni mkoani Tanga Bw. Yibarik Chiza, kulia
akiwaelekeza jambo wakulima wa zao la ufuta wa Kijiji cha Misima
wilayani humo.
Mkuu
wa wilaya ya handeni Bw. Muhingo Rweyemamu, akisalimiana na mmoja wa
wananchi alipotembelea katika kijiji cha Kang’anta kuangalia maendeleo
ya mdada wa mifugo na mazao ya chakula na biashara.
Mmoja
wa wakulima wa nanasi wilayani Handeni Bi Sabrina Rory Sasumua,
akionyesha aina ya nanasi lenye uzito wa kilo mbini na nusu kutoka
katika shambani lake eneo la Kwamsisi wilayani Handeni.
Baadhi ya akina mama wa eneo la Soni katika wilaya ya Lushoto mkoani Tanga wakifanya biashara za matunda na mbogamboga.
Shamba la mahindi katika kijiji cha Manga likionekana kustawi vya kutosha.
(Picha Zote na Mohammed Mhina)
EmoticonEmoticon