NDEGE YA ETHIOPIAN AIRLINE YASHINDWA KUTUA KIA,YALAZIMIKA KUTUA NA KUSIMAMA NJE YA UWANJA WA ARUSHA

December 18, 2013
imewekwa leo desemba 18 saa 7:48 usiku.
Habari zilizoufikia mtandao huu hivi punde kutoka jijini Arusha, zinasema kuwa abiria zaidi ya 200 waliokuwa ndani ya Ndege ya Shirika la Ndege aina ya Boeing 787 ya shirika la ndege la Ethiopia (Ethiopian Airlines) wamenusurika mchana wa leo baada ya ndege hiyo kushindwa kutua kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) kutoka na hitilafu iliyojitokeza kwa dharula Uwanjani hapo na kulazimika kutua kwa dharula kwenye Uwanja wa Mdogo wa Arusha.

Imeelezwa kuwa kutokan na dharula hiyo ndege hiyo imelazimika kusimama nje ya uwanja wa Arusha baada ya kushindwa kusimama kutokana na uwanja huo kuwa mdogo.

Bado Wataalam wa Ndege wapo eneo la tukio wakitafuta namna ya kuwanusuru abiria hao ili kuweza kufungua milango waweze kushuka na kuiwezesha ndege hiyo iweze kuruka tena jambo ambalo bado ni mtihani.
 
taarifa kwa hisani ya Sufianimafotoblog.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »