TIMU ZA HALMASHAURI YA JIJI LA TANGA ZAENDELEA KUTESA SHIMISEMITA

November 01, 2013


Na Twahiru Mdimu ,Dodoma.
MASHINDANO ya Shirikisho za Serikali za Mitaa(Shimisemita) yanayoendelea kutimua vumbi mkoani Dodoma yameingia hatua ya robo fainali huku timu kutoka Halmashauri ya Jiji la Tanga zikiendelea kufanya vizuri katika mashindano hayo.

Timu za Halmashauri ya Jiji la Tanga kutokana na kufanya vizuri katika mashindano hayo leo zimefanikiwa kuingia hatua ya robo fainali ambapo mechi hizo zitaanza majira ya saa nane mchana.

Kwa mujibu wa taarifa zilizoifikia blog ya Tanga Raha zimeeleza kuwa timu ya Halmashauri ya Jiji la Tanga leo jioni itakuwa na kibarua kizito kuweza kuwakabili timu ya Halmashauri ya Mtwara Mikindani kwenye mchezo wa mpira wa miguu.

Katika mchezo mwengine unaotarajiwa kuwa na upinzani wa hali ya juu ni wa pete ambapo timu ya Halmashauri ya Jiji la Tanga watakapowakabiliana wenzao kutoka Halmashauri ya wilaya ya Kyela.

Licha ya kuchezwa mchezo huo kutakuwa na mechi nyengine ambayo itachezwa saa kumi jioni Halmashauri ya wilaya ya Kinondoni watacheza na Halmashauri ya wilaya ya Ulanga kwenye michezo ambao unatazamiwa kuwa na upinzani mkubwa.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »